BARCELONA YAICHAPA HERCULES BILA MSN (MESSI, SUAREZ NA NEYMAR)

Tokeo la picha la ARDA TURAN IMAGE

Arda Turan alipiga Bao 3 wakati Barcelona wakiichapa Timu ya Daraja la 3 Hercules 7-0 na kusonga Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya Copa del Rey kwenye Mechi iliyochezwa Nou Camp Jana Usiku.
 
Licha ya Barca kutoka 1-1 na Hercules katika Mechi ya Kwanza, Kocha Mkuu wa Barca, Luis Enrique, mara baada ya Barca kuitwanga Espanyol 4-1 katika Mechi ya La Liga Juzi Jumapili, aliamua kuwapa likizo ya mapema Mastaa wake Lionel Messi, Luis Suarez, Neymar na Pique likizo kwa vile Soka la Spain litasimama hadi baada ya Wiki ya Pili ya Januari kupisha Sikukuu za Krismasi na Mwaka Mpya.

Bila ya hao Nyota, Barca waliongoza 2-0 hadi Mapumziko kwa Bao za Digne, Dakika ya 37, na Rakitic, ikiwa ni Penati ya Dakika ya 45.
Kipindi cha Pili, Barca waliongeza Bao nyingine kupitia Rafinha, Dakika ya 50, Turan, 55, 86 na 89, na Alcácer, 73     
   
Wakati Timu nyingine Spain zikihenya kufunga Mwaka kwa Mechi hizi za Copa del Rey, Real Madrid wao walicheza mapema Mechi zao za Kombe hili na kufuzu kwa vile walikwenda Japan ambako Juzi walitwaa Kombe la Ubingwa wa Kombe la Dunia kwa Klabu.

 "Real Madrid ilikamilisha Mechi zake na kusonga kwa kuitwanga Cultural Leobesa Jumla ya Mabao 13-2 kwa Mechi 2"

RATIBA YA LEO USIKU MUDA KWA MASAA YA TANZANIA

Alhamisi Desemba 22
22:00  Deportivo Alaves v Gimnastica
    
22:00  Celta de Vigo v UCAM Murcia 
     
23:00  Athletic de Bilbao v Real Racing Santander
      
23:00  RCD Espanyol v Alcorcon  
Tokeo la picha la messi neymar suarez
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment