BAYERN MUNICH YAPAA KILELENI IKIICHAPA RB LEIPZING


Tokeo la picha la philip lahm

MABINGWA WATETEZI Bayern Munich wanaenda kwenye likizo ya Krismasi na Mwaka Mpya wakiwa kileleni mwa Bundesliga baada ya Jana kuibonda Timu iliyopanda Daraja Msimu huu RB Leipzig Bao 3-0.
Sasa Bayern wako mbele ya Timu ya Pili Leipzig kwa Pointi 3.
Bao za Bayern hapo Jana zilifungwa na Thiago na Xabi Alonso na kisha Leipzig wakapata pigo Dakika ya 30 pale Emil Fosberg alipopewa Kadi Nyekundu kwa kumchezea Rafu mbaya Philipp Lahm.      
Robert Lewandowski akapiga Bao la 3 kwa Penati iliyotolewa baada ya Kipa wa Leipzig Peter Gulasci kumchezea Faulo Douglas Costa.
Licha ya kufungwa, kikiwa ni kipigo chao cha pili Msimu huu wao wa kwanza kwenye Bundesliga, Leipzig wako Nafasi ya Pili.
Chini ya Kocha Ralph Hasenhuttl, Leipzig wameshinda Mechi zao 11 za kwanza za Bundesliga kati ta 15 ikiwa pamoja na kuifunga Timu ngumu Borussia Dortmund
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment