FUNGA MWAKA, HULL CITY VS EVERTON ZATOKA SARE.

Tokeo la picha la HULL CITY VS EVERTON IMAGE

Katika mchezo pekee wa ijumaa usiku wa ligi kuu ya Uingereza iliyowakutanisha HULL CITY VS EVERTON ambapo Everton walisawazisha Dakika ya 84 kwa Bao la Ross Barkley na kupata Sare ya 2-2 walipocheza na Hull City huko Kingston Communications Stadium kwenye Mechi pekee ya EPL, Ligi Kuu England.
 Tokeo la picha la ross barkley image
 
Matoke hayo yamewatoa Hull kutoka mkiani na sasa wapo Nafasi ya 19 huku Everton wakibakia Nafasi yao ile ile ya 7.
Hull walitangulia kufunga kwa Bao la Michael Dawson na Everton kusawazisha Dakika za Majeruhi za Kipindi cha Kwanza baada ya Kipa David Marshall kupanchi Mpira wa Kona ya Kevin Mirallas na kutumbukia wavuni.
Frikiki ya Robert Snodgrass iliwapa Hull uongozi wa 2-1 lakini Barkley akawapa Sare ya 2-2.

MAGOLI:
Hull City 2
Dawson 6'
Snodgrass 65'        
Everton 2
Marshall 46', Amejifunga Mwenyewe
Barkley 84'


Leo zipo Mechi 7 za EPL za kufunga Mwaka na mechi ya mwisho kabisa ni ule Mtanange mkali huko Anfield kati ya Liverpool na Manchester City.

VIKOSI:

Hull City: Marshall; Maguire, Dawson, Davies; Elmohamady, Livermore, Meyler, Diomande, Robertson; Snodgrass, Mbokani.
Akiba: Jakupovic, Huddlestone, Clucas, Maloney, Weir, Henriksen, Mason.

Everton: Joel; Coleman, Jagielka, Williams, Baines; Gueye, Barry; Valencia, Barkley, Mirallas; Lukaku.
Akiba: Hewelt, Funes Mori, Holgate, Cleverley, Davies, Lennon, Calvert-Lewin.

REFA: Jon Moss
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment