JE LIVERPOOL ITAISHUSHA NAFASI YA PILI MAN CITY?????

Tokeo la picha la PICHA LIVERPOOL VS STOCK CITY

LEO EPL, Ligi Kuu England, ipo Mechi 1 tu huko Anfield kati ya Liverpool na Stoke City.
Katika Mechi ya mwisho hapo Jana, Man City iliitandika Hull City 3-0 kwa Bao za Yaya Toure, Penati, Iheanacho na Davies aliejifunga mwenyewe.

Liverpool wanashikilia Nafasi ya 3 wakiwa na Pointi 37 sawa na Timu ya 4 Arsenal na kuzidiwa na Timu ya Pili Manchester City Pointi 2 huku Vinara wakiwa Chelsea wenye Pointi 46. Stoke City wapo Nafasi ya 12 wakiwa na Pointi 21.
 
Liverpool wataingia kwenye Mechi hii wakimkosa Majeruhi Philippe Coutinho lakini Beki wao Joel Matip ameshapona na huenda akapewa nafasi.

Kwa Stoke, Fowadi wao Marko Arnautovic bado yupo Kifungoni baada ya kutolewa kwa Kadi Nyekundu kwenye Mechi na Southampton mapema Mwezi huu.

Uso kwa Uso
Liverpool wameshinda Mechi 5 kati ya 6 zilizopita za EPL dhidi ya Stoke na Msimu uliopita kwenye Mechi kama hii walishinda 4-1.

Katika kipindi hicho, Mechi pekee Stoke waliyoshinda ni Bao 6-1 kwenye Mechi ambayo ilikuwa ya mwisho kabisa kwa Nahodha wao maarufu Steven Gerrard.

Pia Stoke walishinda 1-0 Mwezi Januari katika Mechi ya Pili ya Nusu Fainali ya Kombe la Ligi ingawa walishindwa Nusu Fainali hiyo kwa Mikwaju ya Penati Tano Tano zilizopigwa baada ya Mechi 2 za Nusu Fainali kufungana.

VIKOSI VINATARAJIWA KUWA:
LIVERPOOL: Mignolet, Clyne, Lovren, Klavan, Milner, Lallana, Henderson, Wijnaldum, Mane, Origi, Firmino
STOKE CITY: Grant, Johnson, Shawcross, Martins Indi, Pieters, Whelan, Imbula, Diouf, Allen, Krkic, Walters

REFA: Michael Oliver

 Tokeo la picha la PICHA LIVERPOOL VS STOCK CITY

MSIMAMO LIGI KUU UINGEREZA

EPL-DES26B 
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment