WAJUE WALIONG'AA KILELENI KIPINDI CHA KRISMASI..

Tokeo la picha la HAZARD IMAGE
www.kiungomshambuliaji.blogspot.com inakuletea hiiLIGI za Ulaya, mara nyingi sikukuu ya Krismasi hutumika kama kigezo cha dalili za timu fulani kuwa bingwa.

Mfano, timu zilizokuwa kileleni wakati wa Krismasi, asilimia kubwa zilifanikiwa kubeba ubingwa mwishoni mwa msimu. Zipo ambazo ziliboronga mwishoni zikafeli.

Ligi kubwa za Ulaya zina timu 18 hadi 20. Utaona unapofikia msimu wa Krismasi, nyingi ndiyo zinakuwa zimekaribia kumaliza mzunguko wa kwanza ambao unatakiwa kuwa na mechi 19 au 17.

Kwa Tanzania kidogo ni tofauti kwa kuwa kuna timu 16, hivyo hadi inafika Sikukuu ya Krismasi, tayari mzunguko wa pili unakuwa umeanza.

Wakati inafika Krismasi, tayari kila timu imecheza mechi mbili, maana yake kila moja imefikisha mechi 17 na Simba ndiyo wako kileleni wakiwa na pointi 41. Hapa unaweza kuona pia, ile maana ya kipimo cha Krismasi, inaweza kutumika hata hapa nyumbani Tanzania kwa kuwa mara nyingi timu inayokuwa juu hadi kipindi hicho, imetwaa ubingwa ingawa Tanzania kumekuwa hakuna uhakika sana kama ilivyo Ulaya.

Timu nyingi zilishindwa kubeba ubingwa licha ya kuwa kileleni mwa Ligi Kuu Bara inapofikia mwisho wa Desemba kwa kuwa huenda ziliboronga katika mechi zake tano za mwisho ambazo zinakuwa kati ya Aprili na Mei wakati ligi inaisha.


Tanzania Bara:
Simba ina pointi 41 ikiwa inafuatiwa na mpinzani wake namba moja Yanga ambaye ana pointi 37 ikiwa ni pengo la pointi nne sasa baada ya Yanga kulipunguza hadi kufikia pointi mbili tu badala ya nane.

Hadi mechi ya 13, Simba ilikuwa kinara wa ligi, tofauti ya pointi zikiwa ni nane, ikapoteza mechi ya 14 na 15, hivyo Yanga ikasogea na pointi kuwa hizo mbili tu.

Baada ya ushindi wa juzi, Simba imeongeza pengo hadi pointi nne kwa kuwa Yanga ilipoteza hizo mbili baada ya sare ya 1-1 dhidi ya African Lyon baada ya Amissi Tambwe kuisawazishia na bao hilo, halikusaidia kuipeleka kileleni angalau kwa saa chache.
Tokeo la picha la simba fc image

Nafasi ya Simba kubeba ubingwa, huenda si sasa. Wanalazimika kushikilia hivyo hadi watakapokutana na Yanga. Kama watawashinda, basi nafasi itakuwa kubwa zaidi. Kwa mwendo wa ligi ya Tanzania Bara ambayo imejaa makosa ya waamuzi, ujanja wa mipango ya nje uwanja. Si rahisi kusimama na kusema Simba ina nafasi kubwa.

Premier League:
Chelsea imeshikilia kileleni ikiwa na pointi 43, bado mechi mbili imalize mzunguko wa kwanza. Liverpool inaonekana inaifutia kwa kasi kubwa, sasa ina pointi 37.

Chelsea ambao wameshinda mechi 11 zilizopita wako katika kasi nzuri lakini watakaporejea, bado watakuwa na kazi ya kuamsha upya kasi ambayo kama watafanikiwa kumaliza nayo vizuri mzunguko wa kwanza.

Kinachoonekana Manchester City iliyo na pointi 36, bado ni mpinzani wa karibu lakini utaona Arsenal ana 34, Tottenham na 33 na Manchester United amekusanya 30. Hautakiwi hata kidogo kuibeza hata moja kati ya hizo kwa kuwa safari bado ni ndefu sana.


La Liga:
Huku ni mbio za watu wawili, vigogo Real Madrid na FC Barcelona. Mara nyingi akiongezeka atakuwa mmoja Atletico Madrid, Sevilla au Villarreal.

Madrid wako kileleni na pointi 37 lakini wana mchezo mmoja pungufu huku Barcelona wakiwafuatia na pointi 34.

Sevilla wameamka kwenye La Liga safari hii, maana wanaipa Barcelona presha kubwa kutokana na pointi 33 walizokusanya wakiwa na michezo 16 sawa na wao.

Kwa hali inavyokwenda na kiwango cha juu cha Madrid kama watamalizana nacho mzunguko wa kwanza, maana yake watakuwa na kazi ya kukiinua mzunguko wa pili. Wakiteleza, Barcelona, Sevilla hawako mbali.


Bundesliga:
Bayern Munich ni kama wamejimilikisha kombe hilo kwa kipindi kirefu kidogo. Sasa kuna ugumu kwa kuwa RB Leipzig iko nyuma kwa tofauti ya pointi tatu tu.

Bayern wana 36, Leipzig wana 33. Bayern walipata pointi tatu zaidi baada ya kuifunga timu hiyo waliyokuwa wakilingana nayo pointi baada ya kila timu kuwa imecheza mechi ya 15.

Hata kama Bayern imekwenda Krismasi ikiwa kileleni, bado inaonyesha kazi ni ngumu kwa kuwa wao wameshinda mechi zote 5 zilizopita na Leipzig walikuwa wameshinda tano kabla ya wao kuwafunga.

Serie A:
Juventus ambao hawajafungwa mechi tatu zilizopita ndiyo wamekuwa watawala wakuu wa Serie A kwa miaka mitano. Krismasi yao wako kileleni na imekwenda vizuri. Wao wana sifa ya kusimamia vizuri mwenendo wao baada ya kufika kileleni. Wamefanya hivyo kwa miaka mitatu iliyopita.

AS Roma ambao hawajafungwa mechi tisa zilizopita, wako katika nafasi ya pili wakiwa na pointi 38, tofauti ya nne tu na Juventus. Rekodi inaonyesha wamekuwa wakifanya hivyo na mechi tano za mwisho wanashindwa kusimama imara na Juve wanachukua ndoo.Tokeo la picha la kikosi cha juventus image

Ligue 1:
Nice ya Mario Balotelli ndiyo vinara, wana pointi 44 wakiwa wamemaliza mzunguko wa kwanza safi kabisa.

Vigogo Monaco wana pointi 42 katika nafasi ya pili, PSG wana 39 katika nafasi ya tatu. Hakuna ubishi vigogo hawa watakwenda kujipanga.


Nice hawajafungwa mechi 7 zilizopita, Monaco hawajafungwa 4 zilizopita huku PSG wakiwa hawajapoteza hata moja katika mechi 10. Hii inaonyesha mzunguko wa pili, Nice wanalazimika kufunga mkanda hasa hata kama walikula Krismasi, kileleni.
Tokeo la picha la kikosi cha nice ya ufaransa
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment