MUUNGANIKO BORA BAADA YA MZUNGUKO WA KWANZA.

Tokeo la picha la VODACOM PREMIER LEAGUE LOGO 
 
Muunganiko wao umekuwa wa faida ya moja kwa moja klabuni kwa kuzalisha magoli mengi ambayo yamekuwa ndiyo msaada ndani ya timu

Mzunguko wa pili Ligi Kuu Tanzania Bara ulianza wikendi iliyopita kwa timu zote kushuka dimbani kusaka alama tatu muhimu, klabu za Simba na Yanga zimeendelea kuchuana kwa karibu kwenye mbio za ubingwa huku Azam, Kagera na Mtibwa wakikabana koo kwenye nafasi ya tatu na ya nne.

 JKT Ruvu mambo siyo mazuri kwao kwani ndiyo wana kamata mkia kwenye msimamo, Toto Africa, Majimaji na Mwadui hawapo mbali nao kwenye hati hati ya kushuka daraja 
Ukiachana na msimamo wa Ligi, msimu huu zimejitokeza kombinesheni nyingi kwenye klabu ambazo zimezalisha magoli mengi katika michezo 16 tu mpaka sasa na ambayo yamekuwa na faida ndani ya timu zao 

KIUNGOMSHAMBULIAJI inakuletea kombinesheni bora na zilizo zalisha magoli mengi mpaka sasa nusu msimu

Ndiyo muunganiko ulio zalisha magoli mengi Ligi Kuu kuliko zote, Msuva pekee amefunga magoli 9 na kutengeneza magoli  kumi na tatu kwa wenzake huku Niyonzima akifunga goli moja na kuchangia mengine zaidi ya 5
 Tokeo la picha la KICHUYA IMAGE

Wachezaji hawa wa zamani kutoka Mtibwa wamefanikiwa kutengeneza ushirikiano mzuri ndani ya Msimbazi, katika michezo 16 ya Ligi Kuu viungo hawa wamefunga magoli 15, Kichuya amefunga magoli 9 na Muzamiru 6 pia wakitengeneza mengine zaidi ya 7 kwa wengine.

lya Ndanda imefanikiwa kufunga magoli 15 katika michezo 16, katika magoli 15 timu iliyo funga msimu huu asilimia 75  yamefungwa na kombinesheni ya Mponda na Riffat Khamis, washambuliaji hawa kila mmoja ametikisa nyavu mara tano.
 
Chachu ya Mtibwa kufanya vizuri msimu huu ni uwepo wa ushirikiano mzuri kati ya Mandawa na Haruna Chanongo, wamekuwa na msaada mkubwa klabuni, washambuliaji hawa kwa pamoja wamefunga magoli 13, Chanongo magoli 6 huku Mandawa 7
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment