SIMBA KUENDELEA KUIKIMBIA YANGA LEO?

 Tokeo la picha la kikosi cha simba image
Ni mchezo wa ligi ya Vodacom ambao unatabiriwa kuwa kikwazo kwa kikosi cha Simba ambacho kinaongoza ligi kwa tofauti ya pointi MOJA  kati yao na mabingwa watetezi Yanga baada ya mchezo wa Yanga wa jana.
Kikosi cha Simba leo kitakuwa kinarudi tena kibaruani kusaka pointi tatu zitakazoendelea kuwaweka kileleni mwa msimamo wakati watakapo wakabili Maafande wa Ruvu Shooting kutoka Mlandizi mkoani Pwani mchezo ambao umepangwa kupigwa uwanja wa Uhuru Dar es Salaam.

Pamoja na mechi hiyo kupigwa uwanja wa Uhuru, lakini Simba itahesabika kama ipo ugenini kutokana na uwanja unaotumiwa na Ruvu Shooting wa Mabatini uliopo Mlandizi, kutokuwa na usalama wa kuhimili uwingi wa mashabiki watakaoingia kwenye mechi za Simba au Yanga.
Ruvu wanaingia kwenye mchezo huo wakijivunia ushindi wa mabao 2-0, dhidi ya Tanzania Prisons wakati wageni wao Simba nao walipata ushindi wa tabu wa bao 1-0, wakiwa nyumbani uwanja wa Uhuru  dhidi ya Ndugu zao JKT Ruvu.

Maafande hao watataka kushinda mchezo huo ili kuendelea kujiweka sawa kwenye msimamo wa ligi hiyo wakati Simba watahitaji ushindi ili kuzidi kujikita kileleni mwa msimamo wakifikisha pointi 44.
Kocha wa Ruvu Shooting, Malale Hamsini anajua vizuri mziki wa Simba hivyo leo atakuwa na kazi moja ya kuwapunguza kasi Simba wasiendelee kupata matokeo ya ushindi leo.
Malale amesema anaijua Simba pamoja na mbinu zao wanazotumia na yeye atawapanga vizuri vijana wake kuhakikisha wanapata ushindi.
Kocha huyo aliyeifundisha JKT Ruvu mzunguko wa kwanza atakuwa akimtegemea zaidi kiungo Jabir Aziz 'Stima' na mshambuliaji Kisiga ambao wote waliwahi kuichezea Simba siku za nyuma.
Kipa Said Kipao anatarajiwa kukaa langoni na kuwasumbua washambuliaji wa Simba ambao bila shaka wataongozwa na Pastory Athanas , aliyesajiliwa kwenye dirisha dogo akitokea Stand United.
Kwa upande wao Simba maandalizi yao yamekamilika na wana uhakika wa kuendeleza wimbi lao la ushindi kama ilivyokuwa kwenye mechi mbili zilizopita.
 Tokeo la picha la kikosi cha simba image
Kocha Omog, amesema kikosi chake cha leo hakitakuwa na mabadiliko makubwa na kile kilichoanza kwenye mchezo wa JKT Ruvu, na kusisitiza kuwa watacheza kwa umakini mkubwa ili kupata ushindi.
“Hatuwezi kuwadharau Ruvu, kwasababu ni timu nzuri ingawa mchezo wa kwanza tuliwafunga mabao 3-1, lakini  timu yao imekuwa ikibadilika sana na leo lazima tupambane ili kupata pointi tatu,”amesema Omog.
Kiungo Mohamed Ibrahim ‘MO’ anatarajiwa kuanza sambamba na Mghana James Kotei kwenye eneo la kiungo huku kipa mpya Daniel Agyei, akikaa lango ni kwa mechi yake ya tatu kwenye ligi ya Vodacom Tanzania bila kuruhusu bao kwenye nyavu zake.

Mshambuliaji Laudit Mavugo naye anatarajiwa kuanza kikosi cha kwanza baada ya kumaliza dakika 90 za mchezo uliopita akiwa benchi huku Mzamiru Yasini na Shizza Kichuya kwa pamoja wakiwa kwenye eneo ushambuliaji kuwasaidia Mavugo na Pastory.
Kocha Omog, kama kawaida yake amesema atatumia mfumo wa 4-3-3, ili kujaza viungo wengi kwenye eneo la kati lengo likiwa kuwazuia wapinzani wao wasiweze kuipenya ngome yao na kuleta madhara.
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment