PEP GUARDIOLA AKIRI KIWANGO CHA ALEXIS SANCHEZ ALIKITUMIA VIBAYA AKIWA BARCELONA.

 Alexis Sanchez



Hakuna ubishi kwamba Alexis Sanchez ana kipaji cha hali ya juu. Kwa sasa yuko kwenye kiwango bora sana ‘on fire’ tangu alipoachana na Barcelona na kujiunga na Arsenal moto wake umekuwa ni wa hatari sana ndani ya Premier League.

sanchez-vs-pep
                                                 PEP GUARDIOLA NA ALEXIS SANCHEZ

Tangu amekuwa akichezeshwa kama mshambuliaji wa kati na Arsene Wenger, amekuwa akiimarika kila kukicha na kocha wake wa zamani Pep Guardiola amekubaliana na hilo.
Akizungumza kuhusu mchezaji huyo wakati Manchester City inajiandaa kuikabili Arsenal, Pep amekubali kwamba anadhani hakumtumia Sanchez ipasavyo.
“Alicheza vizuri alivyokuwa Barcelona lakini kwa kawaida unapocheza na Messi wachezaji wote huwa hawafikii kiwango chake.”

“Nadhani Arsenal wanamtumia kama striker wa mbele, anafanya vizuri. Tukiwa Barccelona nadhani sikumsaidia vya kutosha kwasababu alicheza pembeni. Anaweza kucheza huko lakini ni bora akacheza mbele karibu na goli.”

 https://encrypted-tbn3.gstatic.com/images?q=tbn:ANd9GcSsnjnXG-JsaskLy32SQLUWcYvvnH4GRigeD2fC24daqJRr5qim

Alexis anafurahia Arsenal lakini kwa sasa yupo kwenye mazungumzo na The Gunners kuhusu mkataba mpya na anataka kuongezewa kiasi cha mshahara ili asaini kkataba mpya kitu ambacho mashabiki wengi wa Arsenal wanasema anastahili.
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment