YANGA KUANZA NA NGAYA CLUB YA COMORO KATIKA CAF CHAMPIONS LIGI 2017

Tokeo la picha la kikosi cha yanga sc


CAF LEO imefanya Droo ya Mashindano ya CHAMPIONZ LIGI kwa Mwaka 2017 na Mabingwa wa Tanzania Bara Yanga wamepangwa kucheza na Ngaya Club ya Comoro katika Raundi ya Awali.
 
Ikiwa Yanga watavuka watatinga Raundi ya Kwanza na kucheza na Mshindi kati ya ZANACO ya Zambia na APR ya Rwanda.

Endapo Yanga watavuka tena hatua hiyo watatua Hatua ya Makundi.
Mabingwa wa Zanzibar, Zimamoto, kwenye Raundi ya Awali, wataanza na Ferroviário Beira ya Msumbiji na Mshindi kutinga Raundi ya Kwanza kucheza na Mshindi wa Mechi ya Barrack Young Controllers ya Liberia na Stade Malien ya Mali.

Tokeo la picha la CAF LOGO

Safari hii Makundi ya CAF CHAMPIONZ LIGI, ambayo sasa Kiudhamini yatajulikana kama TOTAL CAF CHAMPIONZ LIGI, yamepanuliwa toka Mawili ya Timu 8 na kuwa Timu 16 ambayo yatakuwa na Makundi Manne ya Timu 4 kila moja.
Haya ni Mashindano ya 53 ya kusaka Klabu Bingwa Afrika lakini ni ya 21 tangu Mfumo wa CAF CHAMPIONZ LIGI uanze.
Mshindi wa Mashindano haya atafuzu kucheza Mashindano ya FIFA ya Klabu Bingwa Duniani yatakayochezwa Mwaka 2017 huko United Arab Emirates na pia kucheza CAF SUPER CUP dhidi ya Mshindi wa CAF Kombe la Shirikisho.

Bingwa Mtetezi wa CAF CHAMPIONZ LIGI ni Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

1 Maoni: