MASHINDANO
ya Kombe la Mataifa ya Afrika, AFCON 2017, yataanza Jumamosi Januari 14
huko Gabon na kushirikisha Nchi 16 zilizogawanywa Makundi Manne ya Timu
4 kila moja.
AFCON,
ambayo Fainali yake itakuwa Februari 5, itachezwa kwenye Viwanja Vinne
vya Miji ya Libreville, Franceville, Oyem na Port Gentil.
Viwanja
vitakavyotumika ni Stade de l’AmitiĆ©
Stade de l’AmitiĆ© |
huko Libreville, Gabon, unaochukua
Watu 38,000, ambako Kundi A ndio litacheza Mechi zake, na kingine cha
Kundi B ni Port Gentil Stadium, Port Gentil,
Port Gentil Stadium, |
wenye kuchukua Washabiki
20,000, Kundi C lipo Stade de Franceville Mjini Franceville
Stade de Franceville |
wenye uwezo
wa Watu 20,000 wakati Kundi D litakuwa huko Oyem Stadium ulioko Assok
Ngomo,
Gabon, uwezo 20,000.
Oyem Stadium |
Mabingwa
Watetezi wa Afrika ni Ivory Coast lakini safari hii watawakosa
Wachezaji wao wakubwa, wale Ndugu Toure, yaani Yaya na Kolo, ambao
wamestaafu, na Majeruhi Yao Gervinho.
**********************************************
MAKUNDI:
KUNDI A: Gabon, Burkina Faso, Cameroon, Guinea-Bissau
KUNDI B: Algeria, Tunisia, Senegal, Zimbabwe
KUNDI C: Ivory Coast, DR Congo, Morocco, Togo
KUNDI D: Ghana, Mali, Egypt, Uganda
************************************************
Ivory Coast walitwaa Ubingwa wa Afrika huko Equatorial Guinea Mwaka 2015.
Wenyeji Gabon wapo Kundi A pamoja na Burkina Faso, Cameroon na Guinea-Bissau iliyotinga Fainali kwa mara ya kwanza.
Jirani
zetu Uganda wapo kundi D pamoja na Ghana, Mali na Egypt ambao wanarejea
kwenye Fainali hizi kwa mara ya kwanza tangu watwae Ubingwa Mwaka 2010.
0 Maoni:
Post a Comment