AFCON 2017 HIYOO MLANGONI JUA VIWANJA VITAKAVYOTUMIKA.


Tokeo la picha la AFCON IMAGE
MASHINDANO ya Kombe la Mataifa ya Afrika, AFCON 2017, yataanza Jumamosi Januari 14 huko Gabon na kushirikisha Nchi 16 zilizogawanywa Makundi Manne ya Timu 4 kila moja.
 
AFCON, ambayo Fainali yake itakuwa Februari 5, itachezwa kwenye Viwanja Vinne vya Miji ya Libreville, Franceville, Oyem na Port Gentil.

Viwanja vitakavyotumika ni Stade de l’AmitiĆ©
Tokeo la picha la Stade de lā€™AmitiĆ© IMAGE
Stade de l’AmitiĆ©

huko Libreville, Gabon, unaochukua Watu 38,000, ambako Kundi A ndio litacheza Mechi zake, na kingine cha Kundi B ni Port Gentil Stadium, Port Gentil, 
Tokeo la picha la Port Gentil Stadium, IMAGE
Port Gentil Stadium,

wenye kuchukua Washabiki 20,000, Kundi C lipo Stade de Franceville Mjini Franceville 
Tokeo la picha la Stade de Franceville IMAGE
Stade de Franceville

wenye uwezo wa Watu 20,000 wakati Kundi D litakuwa huko Oyem Stadium ulioko Assok Ngomo,
Gabon, uwezo 20,000.
Tokeo la picha la Oyem Stadium IMAGE
Oyem Stadium
Mabingwa Watetezi wa Afrika ni Ivory Coast lakini safari hii watawakosa Wachezaji wao wakubwa, wale Ndugu Toure, yaani Yaya na Kolo, ambao wamestaafu, na Majeruhi Yao Gervinho.
**********************************************

MAKUNDI:
KUNDI A: Gabon, Burkina Faso, Cameroon, Guinea-Bissau

KUNDI B: Algeria, Tunisia, Senegal, Zimbabwe

KUNDI C: Ivory Coast, DR Congo, Morocco, Togo

KUNDI D: Ghana, Mali, Egypt, Uganda

************************************************
Ivory Coast walitwaa Ubingwa wa Afrika huko Equatorial Guinea Mwaka 2015.

Wenyeji Gabon wapo Kundi A pamoja na Burkina Faso, Cameroon na Guinea-Bissau iliyotinga Fainali kwa mara ya kwanza.

Jirani zetu Uganda wapo kundi D pamoja na Ghana, Mali na Egypt ambao wanarejea kwenye Fainali hizi kwa mara ya kwanza tangu watwae Ubingwa Mwaka 2010.

Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment