ARSENE WENGER KUYAKUBALI MASHITAKA YA FA, SASA KIFUNGO KINAMNGOJA!

Tokeo la picha la arsene wenger imaji

Arsene Wenger amethibitisha kuwa atakubali Mashitaka ya FA, Chama cha Soka England, ya Utovu wa Nidhamu yaliyotokana kumkashifu Refa na pia kumsukuma Refa wa Akiba baada ya kuamriwa kutoka nje ya Uwanja na Refa.
 
Jumapili iliyopita kwenye Mechi ambayo Arsenal iliifunga Burnley 2-1, Wenger alimsukuma Refa wa Akiba Anthony Taylor mara tu baada ya kuamriwa na Refa wa Mechi hiyo Jon Moss kutoka nje ya Uwanja kwa kumkashifu ikidaiwa alimwita ‘laghai’.

Wenger alitupwa nje ya Uwanja Dakika ya 93 mara baada ya Burnley kupewa Penati ambayo walisawazisha Bao na Gemu kuwa 1-1 lakini Dakika chache baadae Refa huyo huyo, Jon Moss, ndie aliwapa Arsenal Penati tata na kufunga Bao lao la ushindi katika Dakika ya 98.

Mara baada ya Mechi hiyo, Wenger, mwenye Miaka 67, aliungama na kuomba radhi.

FA ilimpa hadi Leo Alhamisi Saa 3 Usiku, Saa za Bongo, kujibu Mashitaka yake.

Sasa Wenger amesema hatapinga Mashitaka hayo na kuiachia FA impe Adhabu.

Mwaka 2012, Meneja wa Newcastle wakati huo, Alan Pardew, alitwangwa Faini Pauni 20,000 na kufungiwa Mechi 2 kwa kumsukuma Refa Msaidizi, Mshika Kibendera.

Akiongea hapo Jana, Wenger alieleza: “Nipo England kwa Miaka 20 na nimeona mengi na nyinyi mnajua.”

Alipohojiwa kuhusu Adhabu anayotegemewa kupewa, Wenger alisema: “Sitegemei kitu. Niliongea baada ya Mechi ile.”

Licha ya kutoboa kwamba atakubali Mashitaka, Wenger pia alisema ataomba yeye mwenyewe aende kujieleza mbele ya Jopo litakalojadili Kesi yake.

Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment