NAWAOMBA RADHI WASOMAJI WOTE WA BLOG HII YA MICHEZO.

Tokeo la picha la KASSIM OMARY IMAGE
Nawaomba radhi wasomaji wote wa blog hii ya michezo.

Kumekuwa na matatizo makubwa ya upatikanaji wa blog hii kuanzia jana, hali ambayo imetokana na wavamizi wa mtandao kutengeneza virusi vinavyosababisha usumbufu mkubwa kwa wasomaji wakiwatisha kuwa ukiifungua blog hii, kompyuta au simu yako itapata matatizo.

Hali hiyo inaendelea kufanyiwa kazi na wataalamu mbalimbali wakiwemo wale wa Google ambao wamejua kinachofanyika. (Nashukuru Google).

Imani yangu, mambo yatakaa vizuri kuanzia leo au kesho.

Nawaomba radii kwa usumbufu wowote uliojitokeza kwenu na ambao utaendelea kujitokeza.

Kawaida washambulizi hao, huangalia blog zinazosomwa zaidi na kufanya hivyo. Lakini naamini mchango wenu umekuwa mkubwa hadi umewafanya kusikia wivu, lakini juhudi zetu, zitazaa matunda na muendelee kufaidi habari murua za kispoti na burudani kidogo.

Kwa mara nyingine, natoa shukurani kwenu na kuwaomba muendelee kuwa wavumilivu wakati kazi ya marekebisho ikiendelea.

Ahsante

KASSIM OMARY
Founder and Owner of kiungomshambuliaji BLOG.
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment