JAMIE CARRAGHER AHOFIA MSIMU WA LIVERPOOL KUBOMOKA BAADA KUTUPWA NJE NUSU FAINALI EFL CUP!

Tokeo la picha la Jamie Carragher image

MCHEZAJI wa zamani wa Liverpool Jamie Carragher ambae sasa ni Mchambuzi mahiri wa Soka huko England amedai anahofia Msimu wa Liverpool kusambaratika mara baada ya Juzi kufungwa 1-0 na Southampton huko Anfield kwenye Mechi ya Pili ya Nusu Fainali ya EFL CUP na kutupwa nje.
 
Katika Mechi ya Kwanza ya Nusu ya Kombe hilo la Ligi, Liverpool pia ilifungwa 1-0 na Southampton huko Saint Mary.

Tangu Novemba ambapo Kikosi cha Liverpool chini ya Meneja Jurgen Klopp, baada ya kuongoza EPL, Ligi Kuu England, kimekuwa kikiporomoka polepole na sasa wapo Nafasi ya 4 wakiwa Pointi 10 nyuma ya Vinara Chelsea.

Liverpool wameshinda Mechi 1 tu kati ya 7 walizocheza Mwaka huu 2017, na huo ni ushindi wa 1-0 dhidi ya Timu hafifu ya Daraja la Ligi 1 Plymouth waliporudiana kwenye Raundi ya 3 ya FA CUP baada ya Sare yao ya 0-0 huko Anfield.

Mechi zijazo kwa Liverpool ni dhidi ya Wolves kwenye Raundi ya 4 ya FA CUP na kisha na Chelsea kwenye EPL.

Carragher anahisi kipigo chochote kati ya hizo Mechi 2 kitaumaliza kabisa Msimu wao.

Ameeleza: “Wakiendelea kama hivi basi Msimu wao wowote utatoka nje ya Dirisha!”

Gwiji huyo amesema wakishindwa kumaliza nje ya 4 Bora kwenye EPL lawama zote atatupiwa Klopp.

LIVERPOOL – Mechi zijazo:
**EPL isipokuwa inapotajwa

  • 28 Januari – Wolverhampton (FA CUP – Nyumbani)

  • 31 Januari - Chelsea (Nyumbani)

  • 4 Februari - Hull (Ugenini)

  • 11 Februari – Tottenham (Nyumbani)

  • 27 Februari – Leicester City (Ugenini)
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment