EVRA AREJEA KWAO FRANCE, KUKIPIGA MECHI YA KWANZA LEO IJUMAA.

Olympique de Marseille's Patrice Evra poses with his new jersey on January 26, 2017 at the Robert-Louis Dreyfus stadium in Marseille, southern France

MCHEZAJI wa zamani wa Manchester United Patrice Evra anatarajiwa kuichezea Timu yake mpya huko kwao France Marseille wakati wakiikaribisha Montpellier kwenye Mechi ya Ligi 1.
 
Evra, mwenye Miaka 35, ameihama Juventus na kurejea kwao France kujiunga na Marseille ambayo sasa inaimarishwa vilivyo na Mmiliki wake kutoka Marekani, Frank McCourt, ambae ashamsimika Kocha Mpya Rudi Garcia na yupo kwenye harakati kubwa kumsaini Mchezaji wa Kimataifa wa France anaechezea West Ham Dimitri Payet.

Akiongelea kuhusu kuondoka kwa Evra, Kocha wa Juventus Massimiliano Allegri ametamka: “Ni Bingwa mkubwa, Mchezaji wa Kulipwa mwenye kila kitu!”

Hivi sasa Marseille wapo Nafasi ya 7 wakiwa Pointi 15 nyuma ya zile Nafasi za Timu kuichezea UEFA CHAMPIONZ LIGI.

Mbali ya mvuto huo wa Evra, Ligi 1 itavutia zaidi hapo Jumapili wakati Mabingwa Watetezi Paris Saint-Germain wakiwavaa Vinara wa Ligi hiyo kwa sasa AS Monaco.

Baada ya kumnasa Julian Draxler Siku ya Mwaka Mpya, PSG watamkaribisha Straika wa Portugal mwenye Miaka 20 kutoka Benfica Goncalo Guedes.

AS Monaco wanaongoza Ligi 1 wakiwa na Pointi 48 wakifuata Nice wenye Pointi 46 na PSG ni wa 3 wakiwa na Pointi 45.

France -LIGI 1
RATIBA
Leo Ijumaa Januari 27
Marseille v Montpellier

Jumamosi Januari 28
Lyon v Lille
Angers v Metz
Bastia v Caen
Lorient v Dijon
Nancy v Bordeaux
Rennes v Nantes

Jumapili Januari 29
Nice v Guingamp
Toulouse v Saint Etienne
Paris Saint-Germain v Monaco
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment