IJUE TATHMINI YA STOCK CITY VS MANCHESTER UNITED.

 Tokeo la picha la stock city vs man u match preview image
Manchester United watacheza na Stoke City huko Bet365 Stadium leo Jumamosi wakijua fika kuwa bila ya ushindi ndoto zao za kuwemo kwenye mbio za Ubingwa wa EPL, Ligi Kuu England, zinaweza kuyeyuka.
 
Wikiendi iliyopita Man United walitoka Sare 1-1 na Liverpool huko Old Trafford na kudumisha Rekodi yao ya kutofungwa katika Mechi 16 za Mashindano yote.

Vile vile, Man United, chini ya Meneja Jose Mourinho, wameshinda Mechi zao 4 za Ugenini zilizopita na 3 zikiwa za EPL.

Hali za Timu
Wakati Jose Mourinho akiwa na Kikosi kamili cha kuchagua Timu ukimwondoa tu Eric Bailly ambae yuko huko Gabon kwenye Mashindano ya AFCON 2017 na Nchi yake Ivory Coast, Meneja wa Stoke City, Mark Hughes, aliewahi kuichezea Man United Miaka ya nyuma, atawakosa Wachezaji kadhaa akiwemo Kipa wake Jack na nafasi yake kuchukuliwa na Lee Grant.

Vilevile Stoke wana Wachezaji Majeruhi ambao ni Geoff Cameron, Stephen Ireland, Bojan Krkic na Jonathan Walters huku Watatu wakiwa AFCON 2017 na Nchi zao ambao ni Ramadan Sobhi [Egypt], Mame Biram Diouf [Senegal] na Wilfried Bony [Ivory Coast].

Fomu ya Stoke
Baada ya kusuasua, Stoke City hivi karibuni wameanza kupanda Chati na kushinda Mechi zao zote za EPL kwa Mwaka 2017 kwa kuzifunga Watford, wakiwa Nyumbani, na Sunderland, Ugenini lakini kati ya hizo wakatupwa nje ya FA CUP walipofungwa na Wolverhampton Wanderers.

Moja ya sababu ya ushindi wao kwenye Ligi ni fomu ya Straika wao ‘ngongoti’, Peter Crouch, ambae amefunga Bao 3 katika Mechi 3 zao za Ligi zilizopita.
Crouch amebakisha Bao 1 tu kutimiza Bao 100 za Ligi. 

Stoke City vs. Manchester United – Mechi zao za hivi karibuni:
Stoke City
Manchester United
Sunderland 1-3 Stoke City
Manchester United 1-1 Liverpool
Stoke City 0-2 Wolverhamptom
Manchester United 2-0 Hull City
Stoke City 2-0 Watford
Manchester United 4-0 Reading
Chelsea 4-2 Stoke City
West Ham United 0-2 Manchester United
Liverpool 4-1 Stoke City
Manchester United 2-1 Middlesbrough

Kwenye Kikosi cha Stoke City, ukimwondoa Meneja wao Mark Hughes, pia wapo Wachezaji kadhaa ambao walianzia Soka lao huko Man United na hao ni Sentahafu Ryan Shawcross na Fulbeki Phil Bardsley na pia Mame Biram Diouf ambae hayupo kwenye Mechi hii.

Mechi ya Mwisho Kukutana
Mechi ya mwisho kwa Timu hizi kukutana ni huko Old Trafford Mwezi Septemba walipotoka Sare 1-1 kwa Man United kutangulia kwa Bao la Dakika ya 69 la Anthony Martial na Stoke kusawazisha Dakika ya 82 kwa Goli la Joe Allen.

Mechi zilizopita
Hii itakuwa ni Mechi ya 18 kwa Timu hizi kukutana kwenye EPL na Man United kushinda Mechi 8 kati ya 9 Jijini Manchester na kupata ugumu huko Stoke ambako Stoke wameshinda Mechi 2 tu tangu 1984 lakini ushindi huo wa Mechi hizo 2 ni katika Miaka Mitatu iliyopita.

Mara ya mwisho kwa Man United kushinda Nyumbani kwa Stoke ni Mwaka 2013 waliposhinda 2-0 Mwezi Aprili wakiwa njiani kutwaa Ubingwa wa England wakiwa chini ya Meneja wao Lejendari Sir Alex Ferguson.

VIKOSI VINATARAJIWA KUWA:
STOKE CITY [Mfumo 4-2-3-1]: Lee Grant; Glen Johnson, Erik Pieters, Ryan Shawcross, Bruno Martins Indi; Charlie Adam, Glenn Whelan; Joe Allen, Marko Arnautovic, Xherdan Shaqiri; Peter Crouch

MAN UNITED [Mfumo 4-3-3]: David De Gea; Antonio Valencia, Luke Shaw, Phil Jones, Marcos Rojo; Michael Carrick, Ander Herrera, Paul Pogba; Anthony Martial, Henrikh Mkhitaryan, Zlatan Ibrahimovic
Tokeo la picha la Mark Clattenburg image
Mark Clattenburg
 
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment