BIG MATCH ETIHAD STADIUM, JE TOTTENHAM ATAITETEA NAFASI YAKE YA PILI???

Tokeo la picha la man city vs totenham match preview image

ETIHAD STADIUM Jijini Manchester ndio ndimba la Mechi ya mwisho ya Jumamosi Januari 21 ya EPL, Ligi Kuu England, kati ya Manchester City na Tottenham Hotspur, Timu ambazo zipo kikweli kabisa kupigania Ubingwa wa England.
 
City, wako Nafasi ya 5 kwenye EPL wakiwa Pointi 3 nyuma ya Timu ya Pili Spurs ambao wako Pointi 7 nyuma ya Vinara Chelsea.

City wanatinga kwenye Mechi hii wakiwa hali tete baada ya kufungwa Mechi zao 2 kati ya 3 zilizopita na moja ikiwa kisago cha 4-0 toka kwa Everton kiasi cha kumuacha Meneja wao Pep Guardiola akisalimu amri na kusema hawana uwezo wa kutwaa Ubingwa.

Spurs, chini ya Meneja toka Argentina Mauricio Pochettino,tangu wapigwe na Man United Mwezi Desemba, wameshinda Mechi 6 mfululizo za EPL na kukwea hadi Nafasi ya Pili.

Hali za Timu.
Man City sasa wameruhusiwa kumtumia Fowadi Chipukizi hatari wa Brazil Gabriel Jesus baada Uhamisho wake kukwama kutoka Palmeiras ya Brazil licha ya kutua kwao kwa Wiki 3 sasa lakini watamkosa Kiungo Fernandinho ambae yuko Kifungoni.

Spurs watacheza bila ya Beki wao wa kutegemewa Jan Vertonghen ambae sasa imebainika atakuwa nje kwa Wiki 6 baada kuumia Enka.

Walipokutana Uso kwa Uso
  • Tottenham wameichapa City Mechi zote 3 zilizopita na ya mwisho ni 2-0 huko White Hart Lane walipoumaliza mwanzo mzuri wa Pep Guardiola kwenye himaya yake mpya na City Msimu huu.

VIKOSI VINATARAJIWA KUWA:
MAN CITY [Mfumo 4-2-3-1]: Bravo, Sagna, Otamendi, Kolarov, Clichy, Fernando, Toure, Sterling, Silva, De Bruyne, Aguero

TOTTENHAM [Mfumo 3-4-3]: Lloris, Dier, Alderweireld, Davies, Walker, Dembele, Wanyama, Rose, Eriksen, Kane, Alli
Tokeo la picha la Andre Marriner image
Andre Marriner
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment