JOSE FONTE ASAINI WEST HAM UNITED

 Tokeo la picha la Jose Fonte IMAGE
West Ham imemsajili nahodha wa Southampton Jose Fonte kwa kima cha pauni milioni 8 kwa mkataba wa miaka miwili unusu.

Fonte raia wa Ureno mwenye umri wa miaka 33 ambaye aliichezea Southampton kwa miaka saba, aliomba kuihamia West Ham ikiwa imesalia miezi 18 kabla ya mkataba wake kumalizika.

Mkurugenzi wa Southampton Les Reed anasema kuwa Fonte alikuwa na fursa ya kusaini mkataba bora lakini akaomba kuondoka.

Fonte amesema kuwa meneja wa West Ham Slaven Bilic alichangia pakubwa kumshawishi kuichagua West Ham.
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment