Beki
wa kati wa Simba, Juuko Murshid, ameambiwa anatakiwa kurejea mapema
nchini kutoka Gabon alikoenda kushiriki michuano ya Kombe la Afrika
(Afcon) ili ikiwezekana awahi mchezo wa Ligi Kuu Bara kati ya Simba na
Azam FC, kesho Jumamosi.
Juuko
alikuwa akiitumikia Uganda katika michuano hiyo, hivyo kukosa mechi
kadhaa za klabu yake lakini Kocha Mkuu wa Simba, Joseph Omog, amesema
beki huyo anatakiwa kurejea kuendelea na majukumu yake licha ya awali
kuwepo na taarifa kuwa mchezaji huyo hana mpango wa kurejea Simba.
AJIIB NA JUUKO |
“Juuko
wakati wowote anatarajiwa kutua nchini ndani ya wiki hii, ninaamini
kabla ya mechi ya Azam atakuwepo nchini,” alisema Omog.
0 Maoni:
Post a Comment