NGOMA YA WATOTO HAIKESHI, LEO NDIO LEO PALE AMAAN STADIUM

Tokeo la picha la MAPINDUZI CUP IMAGE

LEO zipo Mechi Mbili za Nusu Fainali ya Kombe la Mapinduzi ambayo ni Mashindano ya kuenzi Miaka 53 ya Mapinduzi Tukufu ya Visiwa vya Zanzibar na Pemba, lakini macho, masikio na kila hisia ni Bigi Mechi wakati Dabi ya Kariakoo ikihamia Amaan Stadium Zanzibar kwa Yanga kupambana na Watani zao Simba.
 Tokeo la picha la MAPINDUZI CUP IMAGE
 
Nusu Fainali nyingine hii Leo ni kati ya Watoto wa Nyumbani Taifa Jang’ombe, waliowatoa waliokuwa Mabingwa Watetezi URA ya Uganda, na Azam FC.

Wakati Kambi ya Simba ni shwari baada ya kushinda Mechi 3 na Sare 1 kwenye Kundi A, Yanga kuna walakini baada kushinda Mechi zao 2 za kwanza za Kundi B kwa kishindo na kufuzu lakini wakatandikwa 4-0 na Azam FC katika Mechi yao ya mwisho ya kukamilisha Ratiba Kundini.

Msukukosuko huo umemfanya Kocha Mkuu wa Yanga kutoka Zambia, George Lwandamina, kukiri hali ni ngumu kwao na hasa kutokana na Majeruhi ambao wataikosa Mechi na Simba ambao ni Straika Amissi Tambwe kutoka Burundi, Wazambia wao Wawili, Justin Zulu na Obrey Chirwa, na Mzimbabwe Donald Ngoma. 

 Tokeo la picha la MAPINDUZI CUP IMAGE

Hata hivyo, Kocha huyo amesisitiza wataingia na kupigana kiume kwa Kikosi kilichobaki huku Historia ya Dabi hii ikidhihirisha Miaka nenda rudi Ubora wa Timu si kigezo kwani yeyote anaweza kushinda mtanange kati yao ikiwa Karata zitachangwa vizuri ndani ya Dakika 90 za Mechi.

Yanga na Simba zimekutana Amaan Stadium, Zanzibar mara 4. Pata kumbukumbu:


  • Mechi ya Kwanza 1975
Mwaka 1975, Yanga iliichapa Simba 2-0 kwenye Fainali ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati kwa Bao za Gibson Sembuli na Sunday Manara.

  • Mechi ya Pili 1992
Simba ilishinda Fainali ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati kwa Mikwaju ya Penati 6-5, baada ya Sare ya 1-1 katika Dakika 120 ambayo Simba ilitangulia kufunga kwa Bao la Hussein Masha na Yanga kurudisha kupitia Saidi Mwamba ‘Kizota’,

  • Mechi ya Tatu 1992
Bao pekee la Daniel Kimti liliipa Simba ushindi wa 1-0 katika Nusu Fainali ya Kombe la Muungano.

  • Mechi ya Nne 2011
Simba ilishinda 2-0 kwenye Fainali ya Kombe la Mapinduzi kwa Bao za Shija Mkina na Mussa Hassan ‘Mgosi;.



MSIMAMO:
KUNDI A
NA TIMU P W D L F A GD PTS
1 SIMBA 4 3 1 0 5 1 4 10
2 TAIFA JANG’OMBE 4 3 0 1 6 3 3 9
3 JANG’OMBE BOYS 4 2 0 2 5 5 0 6
4 URA 4 1 1 2 3 3 0 4
5 KVZ 4 0 0 4 2 9 -7 0

KUNDI B
NA TIMU P W D L F A GD PTS
1 AZAM 3 2 1 0 5 0 5 7
2 YANGA 3 2 0 1 8 4 4 6
3 ZIMAMOTO 3 1 0 2 2 3 -1 3
4 JAMHURI 3 0 1 2 0 8 -8 1


Januari 10, 2017

Nusu Fainali
Azam FC v Taifa Jang’ombe (Saa 10: 00 jioni)
Simba v Yanga (Saa 2:15 Usiku)

Ijumaa, Januari 13, 2017
FAINALI
Saa 2: 15 Usiku
Azam FC/Taifa Jang’ombe v Simba/Yanga
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment