MAN CITY WAPATA KIKWAZO JUU YA UJIO WA JESUS.

 Tokeo la picha la GABLIEL JESUS IMAGE

ULE Uhamisho wa Mbrazil Gabriel Jesus kwenda Manchester City bado haujapata Saini ya mwisho ingawa Meneja Pep Guardiola anatarajia utakamilika kabla hawajasafiri kwenda Liverpool Jumapili kucheza na Everton huko Goodison Park kwenye Mechi ya EPL, Ligi Kuu England.

 Tokeo la picha la GABLIEL JESUS IMAGE
 
City walishafikia makubaliano na Klabu ya Brazil Palmeiras tangu Mwezi Julai Mwaka Jana kumnunua Kinda huyo wa Brazil mwenye Miaka 19 kwa Dau la Pauni Milioni 27 na pia kukubali Mchezaji huyo abakie Palmeiras hadi Msimu wa Brazil utakapoisha Mwezi Desemba.
Tokeo la picha la GABLIEL JESUS IMAGE

Jesus amekuwa Kambini na City kwa Wiki 2 sasa lakini ukiritimba umekwamisha Uhamisho wake kukamilika rasmi na hivyo kusitisha kuichezea rasmi City.

Kinda huyo ndio kwanza amechomoza kwenye Soka la Dunia akiwa na Msimu wa Pili tu na Palmeiras lakini akaiongoza Klabu hiyo kutwaa Ubingwa wa Taifa Mwezi Novemba baada ya kutwaa Medali ya Dhahabu akiichezea Brazil kwenye Michezo ya Olimpiki, RIO 2016, Mwezi Julai.

Jesus alianza kukichezea Kikosi cha Kwanza cha Timu ya Taifa ya Brazil Mwezi Septemba Mwaka Jana na kufunga Bao 4 katika Mechi zake 6.

Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment