Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Uganda,Mulitin ‘Micho’ Sredojevic
ameridhishwa na kupangwa kundi moja na timu za Tanzania na Cape Verde
katika michuano ya kufuzu kwa fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika
mwaka 2019.
Lesotho ni nchi nyingine iliyopangwa katika kundi L.
Akizungumza baada ya droo kutolewa, Micho, aliyefanikiwa kumaliza
ukame wa Uganda kufuzu AFCON amesema Uganda wameangukia kwenye kundi
stahili kabisa.
” Tunaweza kuhesabu droo hii kama ni nzuri, hii inathibitisha kazi
nzuri tuliyofanya kwa miaka miwili hadi kupewa droo ya upendeleo. ”
Micho amenukuliwa na mtandao wa Kawowo.
” Ni kundi linalochezeka, tunajua Cape Verde wanashuka kiwango, pia
tunawafahamu ndugu zetu Tanzania. Comoro tuliochezea nao waliwabandua
Lesotho. kiukweli wakati huu tutacheza na timu nyepesi . ”
Mechi za kufuzu AFCON 2019 zimepangwa kuanza mwezi wa Sita huku Tanzania ikianzia nyumbani dhidi ya Lesotho.
0 Maoni:
Post a Comment