SUALA LA JOEL MATIP KUTOCHEZA CAMEROON, FIFA YAITUPIA ZIGO LIVERPOOL.

                   Picha inayohusiana
LIVERPOOL wameambiwa kinagaubaga na FIFA waamue wenyewe kama Mchezaji wao Joel Matip anaweza kuichezea Timu hiyo baada ya kukataa kujiunga na Cameroon kwenye Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika, AFCON 2017, yanayoendelea huko Gabon hivi sasa.
 
Liverpool waliamua wenyewe kumtoa Matip Kikosini Jumapili walipocheza huko Old Trafford na Manchester United kwenye Mechi ya EPL, Ligi Kuu England, wakidai wanangoja ufafanuzi wa FIFA.

Hapo jana FIFA imetoa ufafanuzi na kuitaka Liverpool kufuata Kanuni zinazohusu Wachezaji na moja ikiwa ile inayotaka Mchezaji anaeitwa na Nchi yake kuichezea Timu ya Taifa kutoichezea Klabu yake katika kipindi hicho.

 Tokeo la picha la joel matip image

Liverpool imekuwa ikidai Matip hakuwemo kwenye Kikosi cha mwisho cha AFCON 2017 na kabla alishatangaza kuachana na kuichezea Cameroon.

Hata hivyo, Liverpool wameshindwa kumtumia Matip kwenye Mechi zao na kumwacha Meneja wao Jurgen Klopp akilalamika baada ya Shirikisho la Soka la Cameroon, FECAFOOT, kukaa kimya na kutojibu maombi ya Liverpool ya kutaka ufafanuzi na uthibitisho.

FIFA pia hii Leo imefafanua kuwa Chama cha Soka cha Nchi kikitaka kumwita Mchezaji kwa ajili ya Mashindano ya Fainali za Kimataifa inapaswa kumjulisha Mchezaji anaehusika kwa Maandishi si chini ya Siku 15 kabla Siku anayopaswa kujiunga rasmi na Nchi yake na Taarifa hiyo pia inapaswa kupelekwa kwa Klabu ya Mchezaji huyo katika muda huo huo.
 Tokeo la picha la fifa image

FIFA pia imesisitiza kukiukwa kwa Kanuni hizo kutafanya Wahusika kuburuzwa mbele ya Kamati ya Nidhamu ya FIFA.
Hadi sasa haijulikani kama FECAFOOT ilitoa rasmi Notisi hiyo ya Siku 15 kwa Matip na Liverpool.
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment