PENATI waliyopewa Liverpool hapo Jana huko Old Trafford na kuzaa
Bao lao katika Sare ya 1-1 na Manchester United imezua mjadala na
mabishano makubwa kila kona ya Soka.
Penati hiyo ilitolewa Dakika ya 26 na Refa Michael Oliver kwa madai Paul Pogba alinawa kwa makusudi Kona ya James Milner.
Baada ya Mechi hiyo, Wanahabari walimwandama Meneja wa Man United
Jose Mourinho atoboe ya moyoni kuhusu kutolewa kwa Penati hiyo.
Na Mourinho, ambae Msimu huu amekuwa matatani mara 2 na FA, Chama
cha Soka England, kuhusu kauli zake juu ya Marefa na kushushiwa Faini na
Kifungo, alikuwa mwangalifu mno kuhusu majibu yake.
Mourinho aliwajibu: "Sijui. Sijui. Sikuona lakini Refa alikuwa
karibu pengine ni Penati. Tatizo la Penati si mazingira tu, wakati
mwingine inatolewa, mara nyingine hapana. Inashangaza hizi ni Mechi 19,
21, 21 za Ligi Kuu, pia 3 za Kombe la Ligi na moja ya FA CUP, jumla
Mechi 25, na katika Mechi 25 tumepewa Penati 1 tu.
Lakini leo ilikuwa
kwenye Boksi letu. Sikuiona lakini inabidi niamini ni Penati. Nimefurahi
kuhusu Refa kama ni Penati kwa rekodi yake kwetu Mechi 3 Penati 3 dhidi
yetu!"
Msimu huu, Refa Michael Oliver ametoa Penati 3 dhidi ya Man United kwenye Mechi zao na Watford, Everton na hiyo na Liverpool.
Penati pekee waliyopewa Man United ni kwenye Mechi yao ya Ligi Msimu huu dhidi ya Southampton.
Pia, kwenye UEFA EUROPA LIGI, wakiitwanga Feyenoord walishinda Penati 2.
0 Maoni:
Post a Comment