VINARA
wa La Liga Real Madrid Jana walichapwa 2-1 Ugenini na kuvunjwa mbio zao
za kutofungwa kwa Mechi 40 baada ya Bao la Dakika za Majeruhi la Stevan
Jovetic kuwapa Sevilla ushindi wa 2-1.
Real
ndio waliotangulia kufunga Dakika ya 67 kwa Penati ya Cristiano Ronaldo
iliyotolewa baada ya Dani Carvajal kuangushwa na Kipa wa Sevilla Sergio
Rico.
Dakika ya 85, Sevilla walisawazisha kwa Bao la kujifunga mwenyewe Sergio Ramos na Dakika ya 91 Jovetic kuwapa ushindi Sevilla.
Matokeo
haya bado yamewabakisha Real, ambao walikuwa hawajafungwa tangu Aprili
6, kileleni mwa La Liga wakiwa Pointi 1 mbele ya Sevilla huku Barcelona
wakifuatia wakiwa Pointi 2 nyuma yao lakini Real wamecheza Mechi 1
pungufu kupita Wapinzani wao wote.
0 Maoni:
Post a Comment