BAADA
kuanza kwa Sare katika Mechi 3 za kwanza za Mashindano ya 31 ya
Fainaliza Kombe la Mataifa ya Afrika, AFCON 2017, Senegal imekuwa Nchi
ya kwanza kuzoa Pointi 3 baada ya Jana kuifunga Tunisia Bao 2-0 huko
Port Gentil Stadium, Mjini Port Gentil, Nchini Gabon kwenye Mechi ya
Kundi B.
Juzi, Fainali hizi zilianza kwa Mechi za Kundi A na zote kwenda Sare. Senegal
walitangulia kufunga kwa Penati ya Dakika ya 10 iliyopigwa na Mchezaji
anaechezea Klabu ya Liverpool, Sadio Mane, na kisha kuongeza Bao la Pili
Dakika ya 30 Mfungaji akiwa Kara Mbodji.
Katika
Mechi nyingine ya Kundi B iliyochezwa mapema huko huko Port Gentil
Stadium, Algeria walijinusuru baada ya Mchezaji Bora wa Afrika, Riyad
Mahrez, kuwafungia Bao 2 na kutoka Sare ya 2-2 na Zimbabwe.
Algeria
walitangulia kufunga Dakika ya 12 kwa Bao la Dakika ya 12 la Mahrez
lakini Zimbabwe wakajibu Dakika za 16 na 29 kupitia Kudakwashe Mahachi
na Penati ya Nyasha Mushekwi.
Hata hivyo, Algeria walipata Sare Dakika ya 82 kwa Bao jingine la Mahrez.
Matokeo
ya Mechi hizo mbili za Kundi B yamewafanya Senegal, ambao hawajawahi
kutwaa Ubingwa wa Afrika ila walifika Fainali ya Mwaka 2002 na kutolewa
kwa Penati na Cameroun, wawe kileleni.
Leo zipo Mechi 2 za Kundi C kwa Mabingwa Watetezi Ivory Coast kuanza na Togo
Na kisha Congo DR kucheza na Morocco.
0 Maoni:
Post a Comment