MPUTU AREJEA TP MAZEMBE

Tokeo la picha la MPUTU IMAGE

TP Mazembe imefanikiwa kumrudisha kundini nyota wake wa zamani, Tresor Mputu baada ya kushinda kesi dhidi ya klabu ya Kabuscorp ya Angola.

Mputu alishindwa kucheza kwa muda mrefu baada ya kuondoka Kabuscorp ambayo ilidai amevunja mkataba.

Baada ya juhudi kubwa za rais wa TP Mazembe, Moise Katumbi ambaye alituma wawakilishi wake FIFA, Mputu ameishinda kesi hio na Kabuscorp wameamuliwa kuwalipa TP Mazembe dola milioni 1.5 iliyokuwa ada ya uhamisho wake.

FIFA imeliarifu shirikisho la mpira la JK Kongo, FECOFA kumuidhinisha Mputu kuichezea TP Mazembe kwa mara nyingine.

Mputu anakumbukwa na wengi kwa kuiongoza TP Mazembe kuwa klabu ya kwanza Afrika kufika fainali za Klabu Bingwa Duniani mwaka 2010 walipofungwa na Inter Milan.
 Tokeo la picha la Jonathan Bolingi IMAGE

Kwa upande mwingine, TP Mazembe imewaongezea mikataba nyota wake, Jonathan Bolingi na Rainford Kalaba.


Tokeo la picha la MPUTU IMAGE


Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment