NANI KUBEBA NDOO YA KOMBE LA MAPINDUZI LEO????



Tokeo la picha la simba vs azam image
Fainali za 11 za michuano ya Kombe la Mapinduzi zinatarajiwa kupigwa leo kwenye dimba la Amaan Visiwani Zanzibar kwa kuzikutanisha timu za Simba na Azam zote za Dar es Salaam.

Azam ndiyo ilikuwa timu ya kwanza kutinga hatua hiyo ya fainali kwa kuifunga Taifa Jang’ombe bao 1-0, wakati Simba ilipambana na wapinzani wao wa jadi Yanga na kushinda kwa penati 4-2, baada ya kutoka sare ya bila kufungana katika muda wa kawaida wa dakika 90.

Mchezo huo wa fainali unatarajiwa kuwa na ushindani mkali kutokana na timu hizo kufahamiana vizuri , kutokana na zote kushiriki ligi ya Vodacom Tanzania Bara.

Simba inayotokea kundi A,  katika michuano hiyo inapewa nafasi kubwa ya kushinda mchezo huo kutokana na ubora ambao iliuonyesha katika mechi zake zilizopita ingawa imekuwa na tatizo kubwa kwenye safu ya ushambuliaji.

Kocha wa Simba Joseph Omog, amepania kulitwaa taji hilo, kwa lengo la kuondoa ukame wa makombe ambayo umeikumba klabu hiyo kwa misimu minne iliyopita pasipo kubeba ubingwa wowote.
Tokeo la picha la simba vs azam image

Ukimuondoa beki Juuko Murshind, wachezaji wengine wote wapo kwenye kikosi cha Mcameroon, huyo ambaye ametua Simba msimu huu, baada ya kutimuliwa na Azam misimu miwili iliyopita.

Omog anawajua vizuri wapinzani wake Azam na bila shaka kesho atapanga kikosi imara kwa ajili ya kupata ushindi wa mapema, ili kutimiza adhima yake ya kubeba taji hilo ambalo litakuwa la pili, baada ya mara ya kwanza kuchukua ikiwa na Azam FC.

Kikosi cha Simba hakitarajiwi kuwa na mabadiliko makubwa na kile kilichoanza mchezo uliopita, dhidi ya Yanga na watakuwa wanamtegemea zaidi kipa wao Daniel Angyei, ambaye alidaka penati mbili na kuivusha timu hiyo fainali.

Beki Abdi Banda na Method Mwanjali wanatarajia kuanza kwenye ulinzi wa kati huku Mohamed Hussein na Jamvier Bukungu mfungaji wa penati ya mwisho naye akitarajiwa kuanza kwenye beki wa kuli.

Mshambuliaji Ibrahim Ajibu leo anatarajiwa kucheza mechi yake ya kwanza kwenye mashindano hayo, akianza sambamba na Juma Luizio, ambaye ameonekana akiwa na mchango mkubwa tangu alipoanza kupewa nafasi na kocha Omog, huku wakisaidiwa na Mohamed Ibrahim ‘MO’ na James Kotei kwenye eneo la kiungo.

“Mfumo ambao nitatumia kwenye mchezo wa leo ni 4-3-3 nimeamua kufanya hivyo ili kuwa na watu wengi katikati kwasababu  madhara ya Azam yapo kwenye eneo la kiungo kama unawaacha kutawala unaweza kupata tabu na ndicho kilichowakuta Yanga kwenye mchezo ambao walishinda 4-0,”amesema Omog.

Kwaupande wao Azam kocha wake Idd Cheche, ametamba kuifunga Simba kwa kutumia mbinu zile alizozitumia kwa Yanga, kubeba kombe hilo ikiwa ni muda mfupi tangu kupewa timu.
Tokeo la picha la simba vs azam image

Cheche amesema anatambua kuwa ni mchezo mgumu, lakini wamejipanga vizuri kuhakikisha wanamaliza vizuri michuano hiyo baada ya kuanza vibaya kwa kucheza kiwango kisichoridhisha.

Kocha huyo amesema anaimani kubwa na wachezaji wake kutokana na maelekezo ambayo amewapa na endapo watayafatisha kama alivyowaelekeza anauhakika wa ushindi baada ya dakika 90 za mchezo huo alioupa umuhimu mkubwa kabisa.

Cheche amesema kikosi chake cha leo hakitabadilika kwani, ukilinganisha na kile kilichoanza katika mchezo uliopita dhidi ya Taifa Jang’ombe.

Aishi Manula anatarajiwa  kuanza langoni sambamba na Aggrey Moris na Yakub Mohamed raia wa Ghana na katika safu ya ushambuliaji kocha Cheche itaendelea kuwategemea washambuliaji wake wawili Yahya Mohamed na nahodha wake John Bocco ambaye alifunga bao la kwanza kwenye mchezo dhidi ya Yanga.

Abubakar Salum Sure Boy, anatarajia kuwepo kwenye eneo la kiungo akisaidiana na Frank Domayo mfungaji wa bao lililoivusha timu hiyo kwenye fainali dhidi ya Jang’ombe Jumanne iliyopita.

Vita kubwa katika mchezo huo inatarajiwa kuwa katika eneo la kiungo ambapo James Kotei wa Simba atakapo pambana vikali na Sure Boy na Domayo ambao wameonekana kuwa nguzo muhimu kwa Azam.

Kipa wa Simba anatarajiwa kufanya kazi ya zaida zaidi ya ilivyokuwa kwenye mchezo dhidi ya Yanga kwasababu Azam imeonyesha kuwa na makali kwenye safu yake ya ushambuliaji kwa kuwatumia Bocco na Mohamed.

Wakati kipa wa Simba akitarajiwa kuwa na wakati mgumu Aishi Manula wa Azam yeye anatarajiwa kuwa likizo kwa muda mrefu kutokana na ubutu wa safu ya ushambuliaji wa Simba ambao umekuwa hautishi kama ilivyokuwa timu nyingine kwenye mashindano hayo.
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment