NEYMAR AFUTA UKAME WA BARCA WA MIAKA KUMI DHIDI YA REAL SOCIEDAD.

Tokeo la picha la NEYMAR IMAGE
MESSI NA NEYMAR
UKAME wa kutoshinda Miaka 9 dhidi ya Real Sociedad wakiwa Uwanjani kwao Anoeta Stadium ulimalizika Jana Usiku wakati Penati ya Staa wa Brazil Neymar kuipa Barcelona ushindi wa 1-0 katika Mechi ya Kwanza ya Robo Fainali ya Copa del Rey, Kombe la Mfalme huko Spain.
 
Penati hiyo ilipigwa Dakika ya 21 baada ya Neymar mwenyewe kuangushwa ndani ya Boksi.

Hii ni mara ya kwanza kwa Barca kushinda hapo Anoeta Stadium tangu 2007 na tangu wakati huo Mechi 11 zishapigwa kati yao hapo hapo Anoeta huku Barca wakifungwa 5 na Sare 3 katika Mechi 8 zilizopita.

Mara ya mwisho kwa Barca kushinda, Mwaka 2007, Bao za Andrés Iniesta na Samuel Eto’o ndizo ziliwaibua kidedea.
Msimu huu, kwenye La Liga, Real Sociedad na Barca zilitoka 1-1 huko Anoeta Stadium.

Barca sasa wapo kwenye hatua nzuri ya kutinga Nusu Fainali ya Copa del Rey ambalo wao ndio Mabingwa Watetezi kwani watarudiana na Real Sociedad huko Nou Camp Alhamisi ijayo.

Barca wametinga Nusu Fainali za Copa del Rey kwa Misimu 6 mfululizo hadi sasa wakitwaa Kombe mara 3 na mara 2 kufungwa Fainali.
Fainali ya Copa del Rey ni Mei 27.

Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment