RATIBA LIGI KUU UINGEREZA (EPL)

 Tokeo la picha la epl logo
Ligi Kuu England Ratiba
 
!!!Saa za Bongo!!!  
Jumatatu Januari 2

1530 Middlesbrough v Leicester City               
1800 Everton v Southampton               
1800 Manchester City v Burnley            
1800 Sunderland v Liverpool                
1800 West Bromwich Albion v Hull City           
2015 West Ham United v Manchester United
***************************************
LEO Vigogo wa Soka wa EPL, Ligi Kuu England, Manchester United wanatua huko London Stadium Jijini London kucheza na Timu ngumu West Ham katika Mechi ya Ligi hiyo wakiwa kwenye wimbi tamu la ushindi wa Mechi 5 mfululizo na kutofungwa katika Mechi zao 12 zilizopita.
Tokeo la picha la man u  image

Leo, Jose Mourinho, Meneja wa Man United, anataka kuuanza Mwaka Mpya 2017 kwa mguu mzuri kwa kusaka ushindi dhidi ya West Ham ambayo Msimu uliopita kwenye Mechi kama hii ya EPL kwenye Uwanja wao wa zamani Upton Park walishinda 3-2.

Lakini Msimu huu, Timu hizi zimeshakumbana mara 2 na Man United kutoka 1-1 na West Ham, chini ya Meneja Slaven Bilic, kwenye EPL na Siku 4 baadae kupambana kwenye Robo Fainali ya EFL CUP na Man United kuibuka kidedea kwa Bao 4-1.

Kwenye Mechi hii, Man United itamkosa Beki wao mahiri Eric Bailly ambae Jana aliondoka Kikosini kwenda kujiunga na Timu ya Taifa ya Ivory Coast kwa ajili ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika, AFCON 2017.

Wengine wa Man United ambao hawatakuwepo ni Majeruhi Luke Shaw na wenye hatihati kucheza ni Kepteni Wayne Rooney mwenye maumivu ya Paja na Michael Carrick ambae alikuwa Mgonjwa.

Kwa upande wa West Ham, wana Wachezaji kadhaa ambao ni Majeruhi na hao ni Diafra Sakho, Arthur Masuaku, Alvaro Arbeloa na Gokhan Tore huku wenye hatihati ni Nahodha wao Mark Noble alieumizwa Juzi kwenye Mechi yao na Leicester na kulazimika kubadilishwa na pia wengine wenye hatihati ni Daniel Amartey, Byram na Zaza.

Licha ya upungufu huo, West Ham wameibuka upya hasa baada ya kurejea Kikosini mwao kwa Majeruhi Andy Carroll na Andre Ayew lakini Man United ya sasa, iliyofufuka upya baada ya kucharazwa na Chelsea Mwezi Oktoba si mchezo.

VIKOSI VINATARAJIWA KUWA:

WEST HAM: Randolph, Nordtveit, Reid, Ogbonna, Cresswell, Lanzini, Kouyate, Antonio, Ayew, Payet, Carroll
Akiba kutokana na: Adrián, Spiegel, Feghouli, Zaza, Byram, Fletcher, Calleri, Noble
MAN UNITED: De Gea, Valencia, Jones, Rojo, Darmian, Fellaini, Herrera, Pogba, Rashford, Ibrahimovic, Martial
Akiba kutokana na: Romero, Johnstone, Depay, Fosu-Mensah, Tuanzebe, Schneiderlin, Young, Blind, Schweinsteiger, Lingard, Smalling, Mkhitaryan, Mata, Rooney, Carrick

REFA: Mike Dean
EPL – Ligi Kuu England

Saa za Bongo  
Jumanne Januari 3
2245 Bournemouth v Arsenal                
2300 Crystal Palace v Swansea City                
2300 Stoke City v Watford          
Jumatano Januari 4
2300 Tottenham Hotspur v Chelsea                 
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment