REAL MADRID YACHAPWA MARA YA PILI MFULULIZO COPA DEL REY.

 Tokeo la picha la real madrid image

REAL MADRID Jana wakiwa kwao Santiago Bernabeu wamepokea kipigo chao cha pili mfululizo baada ya kufungwa 2-1 na Celta Vigo katika Mechi ya Kwanza ya Robo Fainali za Copa del Rey, Kombe la Mfalme wa Spain.
 
Real walikuwa kwenye mbio za Mechi 40 za kutofungwa lakini Wikiendi iliyopita zikamalizwa walipochapwa 2-1 na Sevilla kwenye La Liga.
 
Kifungo cha Jana ni mara ya kwanza kwa Real kuchapwa Mechi 2 mfululizo tangu Novemba 2015.
 
Jana Celta Vigo walifunga Bao lao la Kwanza Dakika ya 64 kupitia Iago Aspas aliewahi kuichezea Liverpool na Marcelo kusawazisha kwa bunduki kali Dakika ya 69.
 Tokeo la picha la Iago Aspas image
 
Dakika 1 baadae Celta Vigo wakafunga Bao la ushindi kupitia Castro Otto.
 
 
Picha inayohusiana
 
Timu hizi zitarudiana huko Galicia Jumatano ijayo na Mshindi kutinga Nusu Fainali.
 
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment