VINARA
wa VPL, Ligi Kuu Vodacom, Simba jana wametoka 0-0 na Mtibwa Sugar huko
Uwanja wa Jamhuri Jijini Morogoro na kufyekwa pengo lao na Timu ya Pili
Yanga kuwa Pointi 2 tu.
Juzi Yanga, ambao ndio Mabingwa Watetezi wa VPL, walicheza Ugenini huko
Uwanja wa Majimaji mjini Songea na kutoka na ushindi wa Bao 1-0 dhidi
ya Majimaji FC kwa Bao la mapema la Deus Kaseke na kuikaribia Simba
wakiwa Pointi 1 tu nyuma yao lakini jana pengo hilo limekuwa 2 tu badala
ya 4 walizotegemea Wadau wa Mtaa wa Msimbazi Jijini Dar.
VIKOSI:
MTIBWA SUGAR:
Said Mohamed, Ally Shomary, Issa Rashid ‘Baba Ubaya’, Henry Joseph,
Salim Mbonde, Shaban Nditi, Haruna Chanongo, Ally Makarani, Rashid
Mandawa, Jaffary Salum [Hussein Javu, 84’], Vicent Barnabas [Kevin
Friday, 78’]
SIMBA:
Daniel Agyei, Hamadi Juma, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Method
Mwanjali, Abdi Banda, Jonas Mkude, Shiza Kichuya [Jamal Mnyate, 82’],
James Kotei, Juma Luizio, Laudit Mavugo [Ibrahim Hajib, 54’], Mwinyi
Kazimoto [Pastory Athanas, 75]
MSIMAMO WA LIGI KUU YA VODACOM TANZANIA BARA.
0 Maoni:
Post a Comment