SAGNA, TERRY NA DANIEL AYALA WAKUMBWA NA RUNGU LA PILATO LA FIFA.

Tokeo la picha la BAKARY SAGNA IMAGE
Mchezaji wa Manchester City Bacary Sagna amefunguliwa Mashitaka na FA, Chama cha Soka England, kuhusu Posti yake Mtandaoni Instagram alipohoji umakini wa Refa Lee Mason na wakati huo huo Rufaa ya Nahodha wa Chelsea John Terry atatumikia Kifungo baada ya Rufaa yake kupinga Kadi Nyekundu kutupiliwa mbali.
 
Sagna aliandika kwenye Instagram: “10 dhidi ya 12…lakini tulipigana na tulishinda kama Timu!”

Posti hiyo ilitoka mara baada ya City kuifunga Burnley 2-1 Wiki iliyopita huko Etihad Stadium kwenye Mechi EPL, Ligi Kuu England, ambayo City walibaki Mtu 10 kuanzia Dakika ya 32 kufuatia Kiungo wao Fernandinho kutolewa kwa Kadi Nyekundu na Refa Lee Mason kufuatia Rafu mbaya.

Sheria za FA zinakataza Posti kwenye Mitandao ya Kijamiii zinazohoji uadilifu wa Marefa.
Sagna, ambae ameomba radhi kuhusu Posti hiyo, amepewa hadi Saa 3 Usiku, Saa za Bongo, Ijumaa Januari 13 kujibu Shitaka lake.

WAKATI HUO HUO, Rufaa ya Nahodha wa Chelsea John Terry kupinga Kadi Nyekundu aliyopewa Jumapili walipocheza na Peterborough kwenye FA CUP imegonga mwamba na sasa atatumikia Kifungo cha Mechi 1.
 Tokeo la picha la KADI NYEKUNDU YA JOHN TERRY IMAGE
Adhabu hii itamfanya Terry aikose Mechi ya EPL dhidi ya Mabingwa Watetezi Leicester City hapo Jumamosi.

FA pia imethibitisha Beki wa Middlesbrough, Klabu ya EPL maarufu kama Boro, Daniel Ayala atatumikia Kifungo cha Mechi 3 baada ya Rufaa kupinga Kadi Nyekundu aliyopewa kwenye Mechi ya FA CUP na Sheffield Wednesday Wikiendi iliyopita kutupwa.
 Tokeo la picha la Daniel Ayala IMAGE
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment