SENEGAL YA KWANZA KUFUZU ROBO FAINALI AFCON 2017.

 Tokeo la picha la SENEGAL AFCON2017 IMAGE

SENEGAL Jana wameichapa Zimbabwe 2-0 katika Mechi ya Kundi B la AFCON 2017, Mashindano ya 31 ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika, yanayochezwa huko Nchini Gabon, na kuwa Nchi ya kwanza kutinga Robo Fainali huku wakiwa na Mechi 1 mkononi.
 
Bao zote za Senegal zilifungwa ndani ya Dakika 13 za kwanza huko Mjini Franceville, Gabon kupitia Straika wa Liverpool Sadio Mane na Henri Saivet.
 Tokeo la picha la SADIO MANE AFCON2017 IMAGE

Matokeo hayo, licha ya kuwapeleka Robo Fainali, pia yamehakikisha watamaliza Kundi B wakiwa ndio Nambari Wani hata wakifungwa na Algeria katika Mechi yao ya mwisho.

Nao Tunisia, ambao walichapwa na Senegal 2-0 katika Mechi yao ya kwanza ya Kundi B, Jana waliifunga Algeria 2-1 katika Mechi nyingine ya Kundi B na wanahitaji Sare tu na Zimbabwe katika Mechi yao ya mwisho ili waingie Robo Fainali pamoja na Senegal.

Bao zote za Mechi ya Tunisia na Algeria zilifungwa Kipindi cha Pili na Tunisia walifunga Bao lao la kwanza baada ya Krosi ya Youssef Msakni kutumbukizwa wavuni na Beki wa Algeria Aissa Mandi na la pili kwa Penati ya Naim Sliti iliyotoloewa baada ya Wahbi Khazri kuchezewa Faulo na Faouzi Ghoulam.

Algeria walipata Bao lao pekee Dakika za Majeruhi Mfungaji akiwa Sofianne Hanni.

MSIMAMO WA AFCON 2017:

AFCON-JAN19

Algeria sasa wana kibarua kigumu kufuzu Robo Fainali kwani kwanza wanatakiwa kuifunga Senegal katika Mechi yao ya mwisho na kisha kuomba Zimbabwe iifunge Algeria na hapo ndipo, pengine, wanaweza kufunga kwa Ubora wa Magoli au Tombola ya kurushwa Sarafu.

Leo zipo Mechi 2 za Kundi C kati ya Mabingwa Watetezi Ivory Coast na Congo DR na nyingine ni Morocco na Togo.

Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment