MASHINDANO ya Kombe la Mapinduzi ya kuenzi Miaka 53 tangu Mapinduzi
tukufu ya Visiwa vya Zanzibar na Pemba, ambayo yalianza kwa Mechi
moja ya Kundi A, yameendelea huko Amaan Stadium, Zanzibar kwa Mechi
nyingine mbili za Kundi A.
Katika Mechi ya kwanza Juzi Usiku, Timu pinzani huko Zanzibar zilipambana na Taifa Jang’ombe kuifunga Jang’ombe Boys 1-0.
Katika
Mechi ya kwanza ya hii Leo iliyochezwa mapema, KVZ ya Zanzibar
ilichapwa 2-0 na URA ya Uganda, ambao ndio Mabingwa Watetezi, na Usiku,
Vinara wa VPL, Ligi Kuu Vodacom, Simba, walitinga Amaan Stadium kwa
kucheza na Taifa Jang’ombe.
Katika
Mechi hiyo, Simba walipata Bao la Kwanza Dakika ya 27 ambalo Muzamil
Yasin alifunga na kupiga la Pili Dakika ya 41 Mfungaji akiwa Juma
Luizio.
Dakika ya 76, Lufungo wa Simba alijifunga mwenyewe na kuipa Taifa Jang’ombe Bao na kufanya Gemu iwe 2-1.
0 Maoni:
Post a Comment