WACHEZAJI WA CAMEROON WAKISHANGILIA GOLI LAO LA KWANZA. |
CAMEROON wameingia Fainali ya AFCON 2017, Kombe la Mataifa ya Afrika, baada kuifunga Ghana 2-0 huko Nchini Gabon.
Mechi
hii, Ghana walionekana wako juu kidogo lakini kukosa kwao umakini kwa
nafasi chache walizopata ndio hasa kumesababisha wapigwe.
Frikiki ya Dakika ya 71 ilizaa Bao kwa Cameroon pale Difensi ya Ghana ilipojichanganya na kumruhusu Ngadeu kufunga.
Ndani
ya Dakika za Nyongeza, kaunta ataki ya Cameroon ilizaa Bao lao la pili
kwa Bassogog kuchanja mbuga na Mpira na kumchambua Kipa Brimah na kuipa
Cameroon ushindi wa 2-0.
Sasa
Cameroon watacheza Fainali na Egypt hapo Jumapili kupata Bingwa wa
Afrika wakati Ghana wakicheza Jumamosi na Burkina Faso kusaka Mshindi wa
Tatu.
VIKOSI:
CAMEROON: Ondoa, Oyongo, Fai, Ngadeu, Teikeu, Siani, Djoum, Zoua, Moukandjo, Bassogog, Tambe
GHANA: Brimah; Acheampong, Afful, Amartey, Boye; Wakaso, Acquah, Partey, Atsu, Andre Ayew, Jordan Ayew
AFCON 2017
Ratiba:
**Saa za Bongo**
Mshindi wa 3
Jumamosi Februari 4
2200 Burkina Faso v Ghana
Fainali AFCON 2017
Jumapili Februari 5
2200 Egypt v Cameroon
0 Maoni:
Post a Comment