UEFA CHAMPIONZ LIGI: PEP ASALIMU KWA YAYA, AREJESHWA KUNDINI ULAYA.

Tokeo la picha la YAYA TOURE IMAGE

KIUNGO Yaya Toure amerejeshwa Kikosini mwa Manchester City kwa ajili ya Mechi zao za Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UEFA CHAMPIONZ LIGI, UCL.
 
Toure, mwenye Miaka 33, hakusajiliwa kwa ajili ya Mechi za Makundi za UCL na pia kutupwa nje ya Kikosi cha Kwanza cha Man City baada ya Meneja wa Timu hiyo Pep Guardiola kuingia kwenye Bifu na Wakala wa Gwiji huyo kutoka Ivory Coast.

Wakala Dimitri Seluk alimjia juu Guardiola na Meneja huyo kuapa Toure hatakuwemo Kikosini mwake hadi aombwe radhi.

Wakala huyo hakuomba radhi na ikabidi Yaya Toure mwenyewe achukue jukumu hilo na kuanzia Novemba, Kiungo huyo akarejeshwa Kikosi cha Kwanza.

Kwenye UCL, Toure anachukuwa Nafasi ya Ilkay Gundogan ambae ni Majeruhi.

Man City wataivaa AS Monaco hapo Februari 21 katika Mechi ya Kwanza ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UCL.

UEFA CHAMPIONZ LIGI RATIBA

Raundi ya Mtoano ya Timu 16
**Mechi zote kuanza Saa 4 Dakika 45 Usiku Saa za Bongo**
Jumanne 14 Februari 2017

Benfica v Borussia Dortmund                
Paris Saint Germain v Barcelona   
         
Jumatano 15 Februari 2017
Bayern Munich v Arsenal             
Real Madrid v Napoli     
             
Jumanne 21 Februari 2017
Bayer 04 Leverkusen v Atlético Madrid             
Manchester City v Monaco    
      
Jumatano 22 Februari 2017
FC Porto v Juventus          
Sevilla v Leicester City  
              
Jumanne 7 Machi 2017
Arsenal v Bayern Munich             
Napoli v Real Madrid     
             
Jumatano 8 Machi 2017
Barcelona v Paris Saint Germain            
Borussia Dortmund v Benfica
                
Jumanne 14 Machi 2017
Juventus v FC Porto          
Leicester City v Sevilla 
               
Jumatano 15 Machi 2017
Atlético Madrid v Bayer 04 Leverkusen             
Monaco v Manchester City          
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment