Misri imeweka rekodi kwa kufanikiwa
kufuzu kwa mara ya tisa katika fainali za kombe la Afrika baada ya
kuishinda Burkina Faso 4-3 katika mikwaju ya penalti baada ya sare ya
1-1.
Mlinda lango wa miaka mingi Essam El Hadary alithibitisha
ushujaa wake kwa kuokoa penalti iliopigwa na Betrand Traore ili kupata
ushindi huo.
Wakati wa muda wa kawaida Mohamed Salah aliiweka kifua mbele Misri baada ya kufunga bao zuri.
Hatahivyo Burkina Faso walisawazisha wakati Aristide Bance alipofunga krosi iliopigwa na Charles Kabore.
Kupitia bao hilo Burkina Fasso imekuwa timu ya kwanza kuifunga Misri katika mchuano huo.
Wachezaji
wa Burkinabe ambao ndio walioonyesha mchezo mzuri wakati wa muda wa
kawaida walianza penalti hizo kwa kufunga, lakini Misri ikaibuka mshindi
baada ya Traore kushindwa kucheka na wavu.
0 Maoni:
Post a Comment