MOURINHO ALALAMA 'KUBAGULIWA'!
WAKATI
Timu yake Manchester United ikiipiku Barcelona kwa 'Ubora' huko Ulaya
kwa mwendelezo wa kutofungwa katika Mechi nyingi za Ligi, Meneja wa Jose
Mourinho amelalama kuhusu Marefa kumchukulia yeye tofauti.
Jana kwenye EPL, Ligi Kuu England, Man United ilitoka 0-0 na Hull
City na hiyo ilikuwa Mechi yao ya 14 bila kufungwa kwenye Ligi.
Mara ya mwisho kwa Man United kuonja kichapo ni Oktoba walipofungwa na Vinara wa EPL Chelsea huko Stamford Bridge.
Wimbi hilo limeifanya Man United kuwa kileleni kwenye Ligi 5 kubwa
Barani Ulaya kwa kuongoza kwa kutofungwa katika Ligi kwa muda mrefu
kupita Timu yeyote.
Waliokuwa wakishika hatamu ni Mabingwa wa Spain Barcelona ambao hadi sasa hawajafungwa katika Mechi 13.
Katika Listi hiyo ya Timu za juu Ulaya ambazo hazijafungwa muda
mrefu pia wamo Tottenham ambao wana Mechi 8 za EPL bila kufungwa.
Kwa Ulaya, Timu inayoshikilia Nafasi ya 3 ni Napoli ambayo haijafungwa Mechi 11 za Serie A.
Wakati huo huo, Meneja wa Man United Jose Mourinho amelalamika na
kudai yeye anaamuliwa kwa Sheria tofauti ukilinganisha na Mameneja
wengine wa EPL.
Jana, kwenye Mechi na Hull City, Mourinho alichukizwa na Refa Mike
Jones kwa kushindwa kuwadhibiti Hull waliokuwa wakipoteza muda mno ili
kulinda Sare yao na Mreno huyo kuongea na Refa wa Akiba.
Mourinho ameeleza: "Mnajua wazi mie niko tofauti. Sheria kwangu zipo tofauti."
Aliongeza: "Jana Refa wa Akiba alimwambia Meneja: 'Nafurahia sana
msisimko wako'. Leo mie naambiwa kaa chini au tutakutoa Uwanjani!"
Msimu huu tayari Mourinho ameshatwangwa Vifungo Viwili kutokana na
kuongea kuhusu Refa na pia kupiga Teke Chupa ya Maji akiwa Uwanjani.
0 Maoni:
Post a Comment