Kwa
mujibu wa mmoja wa Wachezaji Magwiji wa Arsenal walioipa Klabu hiyo
Taji lao la mwisho la Ubingwa wa England Msimu wa 2003/04, Meneja wa
Timu hiyo Arsene Wenger hakika atang’oka wakishindwa kutwaa Taji Msimu
huu.
Ray
Parlour, Kiungo mahiri wa Arsenal enzi za ‘Timu isiyofungika’, ameongea
mara baada ya Juzi Usiku Arsenal kuchapwa 2-1 Nyumbani kwao Emirates na
Watford na kuachwa wakiwa Pointi 9 nyuma ya Vinara Chelsea kwenye EPL,
Ligi Kuu England.
Mbali
ya Parlour, pia Washabiki wengi wa Klabu hiyo wanajumuika zaidi na
kuongezeka zaidi Siku hadi Siku kwenye kampeni ya kumtaka Mfaransa
Wenger aliedumu Arsenal kwa Miaka 20 aondoke.
Akihojiwa, Ray Parlour amenena: “Atajua kama hakufanya kazi nzuri Msimu huu na nadhani ataondoka!”
Parlour
pia ametabiri kuwa ikifika wakati wa Wenger kung’oka basi hatakuwa na
uhusiano tena na Klabu hiyo tofauti na Klabu kama Manchester United
wakati Meneja wao wa Miaka 26, Sir Alex Ferguson, alipostaafu akapewa
Ukurugenzi kwenye Klabu hiyo.
Parlour ameeleza: “Sidhani kama atabaki Klabuni. Yeye si Mtu wa aina hiyo!’
0 Maoni:
Post a Comment