Straika
wa Simba, Juma Liuzio, amesema wamejua tatizo lililopo katika kikosi
chao na sasa wanajipanga kufanya kweli katika mchezo wao dhidi ya
Majimaji.
Liuzio
amesema tatizo kubwa katika kikosi chao ni umaliziaji, akidai
wanatengeneza nafasi nyingi lakini umaliziaji ndiyo mbovu, sasa
wameufanyia kazi na wataanza kuonyesha mabadiliko hayo katika mechi ya
Majimaji.
“Sidhani
kama Simba ni timu mbovu kama watu wanavyofikiri, nikwambie kitu, sisi
washambuliaji tungekuwa makini mechi na Azam, basi matokeo
yasingemalizika yale ya kufungwa bao 1-0.
“Kiukweli,
viungo wetu walitutengenezea nafasi nyingi za kufunga lakini umakini
wetu mbaya ndiyo ukasababisha sisi tupoteze mchezo huo.
“Tumeliona
hilo tatizo letu, niwaahidi mashabiki wa Simba kuwa, tatizo hilo
tumelimaliza na mechi dhidi ya Majimaji tutathibitisha hilo,” alisema Liuzio.
0 Maoni:
Post a Comment