MOURINHO: WACHEZAJI WENYE UBINAFSI WALIMSALITI RANIERI.

Mourinho asema wachezaji wa Leicester walimasliti Ranieri

Mkufunzi wa Manchester United Jose Mourinho amewashutumu wachezaji wa Leicester kwa kuwa na ubinafsi wa kumsaliti aliyekuwa mkufunzi wao Claudio Ranieri.

Mkufunzi huyo alivaa kofia yenye nembo za CR akimuunga mkono Claudio Ranieri kabla ya kuwashutumu wachezaji hao ambao wengi wao walisaini kandarasi mpya baada ya kushinda taji la ligi.

Muorinho alifutwa kazi katika mandhari kama hayo msimu uliopita kufuatia mgomo wa wachezaji lakini akasema kuwa kisa alichofanyiwa kilikuwa kidogo sana ikilinganishwa na vile Ranieri alivyofanyiwa.

''Nadhani msimu huu ulianza na ubinafsi mwingi wachezaji wakitaka kupewa mikataba mipya'' .

''Watu wakifikiria fedha zaidi wengine wakiamua kuondoka bila kujali ni nani aliyewafanya kufikia walivyo'' alisema Mourinho.
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment