EPL: LEO MAN UNITED KUPAA HADI NAFASI YA 4?

Tokeo la picha la MAN U VS BOURNEMOUTH MATCH PREVIEW IMAGE

MANCHESTER UNITED Leo inatinga Uwanja wao wa Nyumbani Old Trafford kucheza Mechi yao ya EPL, Ligi Kuu England, na Bournemouth wakiwa na uwezo wa kupanda hadi Nafasi ya 4 wakishinda lakini Meneja wao Jose Mourinho ametangaza lengo lao sasa ni kumaliza Nafasi ya Pili Msimu huu.
 
Man United hawajafungwa katika Mechi 16 za EPL na sasa wapo Nafasi ya 6 wakiwa Pointi 15 nyuma ya Vinara Chelsea kitu ambacho Mourinho ameona kuutamani Ubingwa Msimu huu ni kitu kisichowezekana lakini kwa Nafasi ya Pili inawezekana kwa vile Tottenham, walio Nafasi ya Pili, wapo Pointi 5 mbele yao.

Jana Mourinho ameeleza: “Nafasi ya Pili ni ngumu lakini inawezekana. Ya Kwanza haiwezekana ila ya Pili inawezekana na inabidi tuipiganie!”

Aliongeza: “Halafu tupiganie EUROPA LIGI nayo ni ngumu lakini tupo kwenye Tiumu 16 za mwisho! Kwa sasa tunacheza na Bournemouth, tunacheza na Chelsea [FA CUP Robo Fainali] na tunacheza na Rostov [EUROPA LIGI], na kisha tutaona tuko wapi.”

Kuhusu Mechi ya Leo, Man United itamkosa Henrik Mkhitaryan ambae anasumbuliwa na Misuli ya Pajani wakati Bournemouth Majeruhi wao ni Francis, Wilson na Federici.
Bournemouth wako katika hali tete na hawajashinda Mechi yeyote ya Mashindano yote katika Mechi 8 zilizopita.

Mara ya mwisho wao kushinda ni Tarehe 31 Desemba 2016.
Mara ya mwisho kwa Bournemouth kuivaa Man United ni Mwaka Jana Agosti 14 kwenye Mechi ya ufunguzi ya Msimu mpya wa EPL huko Vitality Stadium na Man United kushinda 3-1 kwa Bao za Juan Mata, Wayne Rooney na Zlatan Ibrahimovic huku Adam Smith akiipa Bournemouth Bao lao.

VIKOSI VINATARAJIWA KUWA:
MAN UNITED: De Gea, Valencia, Smalling, Bailly, Blind, Carrick, Herrera, Mata, Pogba, Rashford, Ibrahimovic
Akiba kutokana na: Subs from Pereira, Fosu-Mensah, Tuanzebe, Young, Schweinsteiger, Lingard, Rojo, Romero, Rooney, Shaw, Darmian, Martial, Fellaini

BOURNEMOUTH: Boruc, Cook, Mings, Daniels, Arter, Surman, Stanislas, Wilshere, Fraser, King
Akiba kutokana na: Allsop, Jordan, B Smith, Cargill, Mousset, Gosling, Ibe, Pugh, Ramsdale, Gradel

 Tokeo la picha la Kevin Friend IMAGE
                                REFA: Kevin Friend
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment