EPL: LEO USIKU ANFIELD NI KIMBEMBE LIVERPOOL NA ARSENAL.

  Tokeo la picha la LIVERPOOL VS ARSENAL MATCH PREVIEW IMAGE

USIKU huu huko Anfield Jijini Liverpool, Wenyeji Liverpool wanatinga kucheza na Arsenal kwenye Mechi ya EPL, Ligi Kuu England, inayokutanisha Timu ambazo zipo Nafasi za 4 na 5.
 
Arsenal wako Nafasi ya 4 wakiwa na Pointi 50 kwa Mechi 25 na Liverpool ni wa 5 wakiwa wamecheza Mechi 26 na wana Pointi 49.

Mechi hii ni ngumu hasa ukiangalia Takwimu zake kwani Liverpool wameshinda Mechi 1 tu wakiwa kwao Anfield katika 9 zilizopita na hiyo ilikuwa 5-1 Februari 2014 na nyingine kwenda Sare 5 na Kufungwa 3.

Lakini mapema Msimu huu, kwenye EPL huko Emirates Jijini London, Liverpool iliinyuka Arsenal 4-3 hapo Agosti 14 kwa Bao za Coutinho, Bao 2, Lallana na Sadio Mane huku Arsenal wakifunga kupitia Theo Walcott, Oxlade-Chamberlain na Chambers.

Mbali ya ugumu wa Mechi yenyewe, pia hata Mameneja wa Timu hizi mbili nao wako kwenye presha kubwa.

Jurgen Klopp sasa ameanza kupondwa waziwazi na Mashabiki wa Liverpool hasa baada ya Jumatatu iliyopita kuchabangwa Bao 3-1 na Mabingwa Watetezi Leicester City huko King Power Stadium na kuonyesha kupoteza mwelekeo kwenye EPL.

Nae Arsene Wenger, hasa baada ya kudundwa 5-1 na Bayern Munich kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI huko Munich, huku pia akipoteza mwelekeo kwenye EPL hasa kipindi hiki kama kawaida yao, amekuwa akisakamwa ang’oke.

**************************************
JE UNAIJUA HII?
  • Arsène Wenger ataingia kwenye Gemu yake ya 50 dhidi ya Liverpool na Leo anapigana asifungwe na Liverpool kwa mara ya Pili katika Msimu mmoja wa EPL kitu ambacho mara ya mwisho kilitokea Mwaka 2000.
**************************************

Kwenye Gemu kama hii ya EPL iliyochezwa Anfield Msimu uliopita, Timu hizi zilitoka Sare ya 3-3.

Majeruhi
  • Liverpool: Ings, Ejaria, Sturridge na Henderson [Huenda akacheza].
  • Arsenal: Elneny na Cazorla

VIKOSI VINATARAJIWA KUWA:

LIVERPOOL: Mignolet, Clyne, Matip, Lovren, Milner, Lallana, Can, Wijnaldum, Mane, Firmino, Coutinho

Akiba watatokana na: Karius, Manninger, Origi, Klavan, Moreno, Stewart, Henderson, Randall, Alexander-Arnold, Woodburn, Ojo, Wilson, Gomez, Henderson, Lucas

ARSENAL: Cech, Bellerin, Mustafi, Koscielny, Monreal, Oxlade-Chamberlain, Coquelin, Xhaka, Welbeck, Sanchez, Ozil

Akiba watatokana na: Ospina, Martínez, Jenkinson, Debuchy, Mertesacker, Gabriel, Holding, Gibbs, Ramsey, Maitland-Niles, Iwobi, Reine-Adélaïde, Sanogo, Walcott, Pérez, Giroud.

 Tokeo la picha la Robert Madley IMAGE
        REFA WA MCHEZO HUO: Robert Madley
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment