JE LEO ARSENAL KUIAGA RASMI ULAYA?

Tokeo la picha la ARSENAL VS BAYERN MUNICH MATCH PREVIEW IMAGE

KWA MARA NYINGINE tena Arsenal wanachungulia kutupwa nje ya Hatua ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGI, hatua ambayo mara ya mwisho waliivuka Msimu wa 2009/10.
 
Kibarua kigumu cha Arsenal kinatokana na kuchapwa 5-1 na Wababe wa Germany Bayern Munich kwenye Mechi yao ya Kwanza iliyochezwa Allianz Arena huko Munich.

Ili kusonga Robo Fainali, Arsenal wanahitaji ushindi wa 4-0 au matokeo mengine ili mradi tofauti ya Magoli ibakie 4-0 kwa upande wao.

Kazi hii ngumu ipo ngumu zaidi kwao kwa vile pia watamkosa Kiungo wao Mjerumani Mesut Ozil ambae ni Mgonjwa.

Lakini Arsenal wanaweza kumtumia kwa mara ya kwanza Sentahafu wao Mjerumani Per Mertesacker ambae ni Kepteni wao baada ya kupona Goti na hii itakuwa Mechi yake ya kwanza kucheza Msimu huu ikiwa atacheza.

Pia huenda Meneja wa Arsenal Arsene Wenger huenda akamuanzisha Fowadi wao kutoka Chile Alexis Sanchez ambae hakuanza Jumamosi iliyopita walipotwangwa 3-1 na Liverpool huko Anfield kwenye Mechi ya Ligi Kuu England baada kuvumishwa kulikuwa na rabsha Mazoezini iliyomhusu yeye.

Sanchez ndie Mfungaji Bora wa Arsenal Msimu huu akiwa na Bao 20.
Kwa upande wa Bayern Munich, chini ya Kocha Mtaliano Carlo Ancelotti, itawakosa Jerome Boateng ambae ni Majeruhi na Philipp Lahm ambae yupo Kifungoni.


JE WAJUA KUELEKEA MECHI YA ARSENAL VS B. MUNICH?
  • Arsenal na Bayern zimekutana mara 11 na 7 kati ya hizo ni katika Miaka Minne iliyopita.
  • Bayern imeshinda Mechi 6 na kufungwa 3 tu kati ya hizo huku wakiipiga Arsenal 5-1 mara 2 mfululizo katika Mechi 2 zilizopita.

Pengine matumaini makubwa kwa Arsenal ni kuwa Bayern imepigwa mara 2 mfululizo kila walipotua England katika Mechi 2 zilizopita na ya mwisho ikiwa Emirates walipochapwa 2-0 na Arsenal kwa Bao za Olivier Giroud na Mesut Ozil.

Lakini Bayern watatua Emirates wakiwa hawajafungwa katika Mechi 16 huku wakishinda Mechi 14 kati ya hizo mbio zilizoanzia Novemba Mwaka Jana.

Katika Mechi zao 5 zilizopita, Bayern wamenyuka Bao 20.
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment