KOCHA MBEYA CITY ANAAMINI SASA WATAAMKA NA KUFANYA KWELI.

Tokeo la picha la MBEYA CITY IMAGE

Kocha Mkuu wa Mbeya City, Kinnah Phiri ameendelea kusisitiza kuwa kikosi chake sasa kina nafasi ya kuamka na kufanya vema.

Baada ya sare ya mabao 2-2 dhidi ya Simba huku Mbeya City ikionyesha soka safi, Phiri raia wa Malawi amesema anaamini kikosi chake kitafanya vema.

“Morali imepanda na si kwamba wachezaji hawanielewi lakini mchezo wa soka unajumuisha mambo mengi sana,” alisema.

“Sasa ninaamini wataweza kucheza kwa kiwango hicho na baada ya hapo kuendelea kukipandisha,” alisema.

Kabla, Mbeya City ilikuwa inasuasua kwa kiasi kikubwa licha ya juhudi ya usajili mzuri.
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment