JE UHUSIANO WA SOKA KWA WENGER ULIODUMU KWA MIAKA MINGI UNAFIKIA KIKOMO?

  Tokeo la picha la wenger image

Arsene Wenger, ameihudumia kama meneja wa klabu ya Arsenal kwa miaka 21 lakini wiki hii imeweka hatma yake ya miaka ijayo katika wasiwasi kuliko wakati mwengine ule wowote katika uongozi wake.

Kubanduliwa kwa mara ya saba katika hatua ya kumi na sita bora katika ligi ya kombe la vilabu bingwa Ulaya ulikuwa uchungu wa kutosha, bila kuongeza pigo la magoli 10-2 kutoka kwa Bayern Munich.

Malalamiko dhidi ya Wenger yamekuwa yakisikika chini kwa chini kwa miaka mingi lakini sasa malalamiko hayo yameongezeka .

Kwa mwaka huu wote, mkataba mpya bado uko mezani, huku meneja huyo mwenye umri wa miaka 67 akisema maoni ya mashabiki yatachochea uamuzi wake iwapo atasalia kama meneja.

Wenger kila mara hukosolewa na vyombo vya habari, na mashabiki wengi wamezoea kupata habari na mabadiliko na sio uthabiti wake.

Alisema maneno sawa na hayo yeye mwenyewe .

Liverpool hawajawahi shinda ligi ya Uingereza na Manchester United wamechukua muda tangu kushiriki katika ligi ya Vilabu bingwa Ulaya lakini wawili hao wamekuwa na zaidi ya mameneja mmoja ndipo hawakosolewi mara nyingi.
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment