KUKOSA NAMBA KIKOSI CHA KWANZA, MANYIKA JR KUONDOKA SIMBA MWISHONI MWA MSIMU HUU

  Peter Manyika
Manyika anatarajiwa kuondoka Simba baada ya baba yake kumwahidi kumtafutia timu nyingine sababu ya kukosa nafasi kwenye kikosi cha Simba.
 
Kipa namba mbili wa Simba Manyika Peter huenda akaachana na timu hiyo mwishoni mwa msimu huu baada ya Baba yake kumtaka kutafuta timu ambayo atapata nafasi ya kucheza.
 
Manyika amesema kuwa amevumilia kwa muda mrefu lakini kwa sasa amepoteza matumaini kutokana na maisha yake yote kuishia benchi jambo ambalo lina mvunja moyo wa kuendelea kuichezea timu hiyo akihofia kupoteza kipaji chake.
 
“Baba amenishauri mwishoni nitafute timu nyingine ya kuchezea, kwa sababu kuendelea kubaki Simba ni sawa na kuua kipaji changu, muda mwingi nakuwa benchi hata kwenye mechi za kirafiki kipa anayepangwa ni Mghana Daniel Agyei,” amesema Manyika.
 
Kipa huyo amesema anafikiria kutekeleza ushauri wa mzazi wake kwa sababu nikweli, kiwango chake kimekuwa kikipungua siku hadi siku jambo linasababishwa na kutocheza mechi za ushindani ukiacha mazoezini.
 
Amesema kama mchezaji mdogo anandoto za kufanya vizuri na kwenye nafasi hiyo ya langoni lakini anashangazwa na maboss zake Joseph Omog na msaidizi wake Jackson Mayanja kumfungia vioo huku wakimsotesha benchi.
 
“Inauma kuona msimu umebakiza mechi sita alafu sijacheza hata mechi moja na mbaya zaidi wageni wanakuja na kupata nafasi huku mimi nikiendelea kuwa mchezaji wa mazoezini kwani hata mechi za Kombe la FA au zile za kirafiki sipangwi,” amesema Manyika.
 
Kipa wa zamani wa Yanga na Taifa Stars, Peter Manyika, amesema atamwondoa mwanawe, Manyika Peter, kudakia Simba kutokana na kukosa nafasi katika kikosi cha kwanza cha Joseph Omog.
 
Manyika alijiunga na Simba kwa mkataba wa miaka miwili ambao unamalizika mwishoni mwa msimu huu na tayari baba yake mzazi Peter Manyika ambaye amewahi kuichezea timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ na klabu ya Yanga amemhakikishia kumtafutia timu ya kucheza itakayompa nafasi ya kikosi cha kwanza.
 
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment