LA GALAXY KUMTAJIRISHA IBRAHIMOVIC

  Galaxy

Uongozi wa klabu ya LA Galaxy ya marekani umedai kwamba kwa sasa una mpango wa kumnunua mshambuliaji wa Manchester United Zlatan Ibrahimovic kwa dau kubwa liltakalo mfanya awe ndio mchezaji ghali zaidi wa kulipwa katika Ligi Kuu ya soka ya marekani.

Ibrahimovic alijiunga na United kwa mkataba wa mwaka mmoja msimu mfupi uliopita.

Lakini hata hivyo ni maamuzi ya hiari kwa msweeden huyo ya kuchagua kuondoka au kubakia endapo United watahitaji kufanya mazungumzamo na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka kwa 35.

Mpaka sasa Ibrahimovic aimefunga mabao 26 United katika msimu huu, leo Alhamisi atakosa mchezo wa Uefa Europa ligi dhidi ya Rostov kutokana na kutumikia adhabu ya mechi tatu hii ni baada ya kuadhibiwa kutokana na makosa aliyoyafanya kwenye mchezo dhidi ya Bournemouth kwa kumchezea madhambi Tyrone Mings siku ya Jumamosi iliyopita katika uwanja wa Old Traford.

Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment