MAURICIO POCHETTINO: ASEMA HAWEZI KUWA MKUFUNZI BARCELONA.

Mauricio Pochettino
Mauricio Pochettino alikuwa meneja wa Espanyol kati ya 2009 na 2012
Meneja wa Tottenham Mauricio Pochettino amedokeza kwamba "haiwezekani" kwake kuwa meneja wa klabu ya Barcelona ya Uhispania.

Mkufunzi huyo wa zamani wa klabu ya Espanyol alikutana na rais wa Barca Josep Maria Bartomeu wiki iliyopita huku uvumi ukiongezeka kwamba huenda akamrithi Luis Enrique.

Hata hivyo, BBC imefahamu kwamba yeye si miongoni mwa wanaotathminiwa kwa ajili ya kupewa kazi hiyo.

"Mimi ni shabiki wa Espanyol - Nafikiri sihitaji kusema sana kuhusu hilo," raia huyo wa Argentina alisema, akisisitiza uhasama kati ya Espanyol na majirani zao wa jiji Barcelona.

Pochettino, 45, pia alichezea Espanyol mechi 216.
Katika kikao na wanahabari Alhamisi Pochettino alisema:

 "Ni kama siku moja, iwapo (mwenyekiti wa Spurs) Daniel Levy atanifuta kazi, haiwezekani kwangu kuwa mkufunzi wa BARCELONA."
Taarifa zinasema Spurs walifahamu kuhusu mkutano wa POchettino na rais huyo wa Barca.

Mkufunzi msaidizi wa Barca Juan Carlos Unzue anapigiwa upatu kumrithi Enrique ambaye anaondoka mwisho wa msimu.

Mkufunzi wa Athletic Bilbao Ernesto Valverde pia anaaminika kuwa miongoni mwa wale ambao wanaweza kupewa kazi hiyo.
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment