UEFA CHAMPIONZ LIGI: NI HISTORIA, BARCA 'YAFUFUKA', YATWANGA 6 NA KUSONGA.

 Tokeo la picha la BARCELONA TEAM IMAGE

MABINGWA wa Spain FC Barcelona Jana waliweka Historia mpya baada ya kutinga Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONZ LIGI, UCL, kwa kishindo kikuu walipoitwanga Paris Saint Germain huko Nou Camp Jijini Barcelona.

Barca walichapwa 4-0 na PSG katika Mechi ya Kwanza ya Mtoano ya Timu 16 Wiki 3 zilizopita huko Paris na haijapata kutokea katika Historia ya UCL kwa Timu kupindua kipigo hicho na kusonga.
 
Lakini Jana Barca walivunja mwiko huo kwa Bao za Luis Suárez (3'), Kurzawa (40', kajifunga mwenyewe), Messi (50', Penati), Neymar (88' na 90'+1 Penati), Sergi (90'+5 ).
 
Bao pekee la PSG lilifungwa na Edinson Cavani katika Dakika ya 62. Kwa Matokeo hayo Barca imesonga kwa Jumla ya Mabao 6-5 kwa Mechi 2.
 

Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment